Machapisho

Kombe la FA England labadilishwa jina

Picha
Michuano mikongwe barani Ulaya ya kombe la FA sasa imefikisha miaka yake 144 tangu kuanzishwa kwake, Habari mpya kutoka ndani ya bodi ya kombe la hilo la FA ni kwamba kwa sasa

Kaseja, Mgosi watoa mapya kuhusu Simba

Picha
WAKATI kukiwa na tetesi za Simba kutaka kuwarudisha kundini wachezaji wake wa zamani Juma Kaseja na Mussa Hassan ‘Mgosi’ ili kuimarisha kikosi chao msimu ujao, wachezaji hao kila mmoja ametoa lake la moyoni.

TFF yatembeza adhabu kali Ligi Kuu

Picha
MWAMUZI wa mechi kati ya Azam FC na Kagera Sugar, Stephen Makuka na msaidizi wake namba mbili Said Mnonga wameondolewa kwenye orodha za waamuzi wa Ligi Kuu na kufungiwa kwa muda wa mwaka mmoja baada ya kushindwa kumudu mchezo huo. Meneja wa Kagera Sugar, Mohamed Hussein anapelekwa kwenye Kamati ya Nidhamu ya TFF kwa kutoa lugha ya matusi kwa waamuzi na kutaka kumpiga mwamuzi msaidizi namba 2, Said Mnonga kwenye mechi namba 158 dhidi ya Azam FC iliyochezwa Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto adhabu hiyo imetolewa kwa kuzingatia Kanuni ya 38(1) ya Ligi Kuu. Katika mechi hiyo Azam iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 ambapo hata hivyo Kagera walikuwa walilalamikia bao la pili lililofungwa na Gaudence Mwaikimba kuwa

Owino yuleee Yanga

Picha
George Owino WAKATI mashabiki wa Simba wakiendelea kuugulia maumivu ya kuondokewa na mfungaji wao bora wa msimu uliopita, Amis Tambwe huenda wakalia zaidi baada ya Yanga kuwa kwenye mikakati mizito ya kumsajili beki la nguvu la timu hiyo Mganda, Joseph Owino. Owino anamaliza mkataba wake ligi itakapomalizika Mei mwaka huu ambapo taarifa za uhakika kutoka kwa kigogo mmoja wa Kamati ya Usajili ya Yanga zinaeleza kocha Mkuu wa Klabu hiyo, Hans Van de Pluijm anataka saini ya Owino ili kuimarisha safu yake ulinzi. Tangu kuwasili kwa kocha wa sasa wa Simba, Goran Kopunovic, Owino amekuwa akisugulishwa benchi na kusubiri hadi aumie kati ya Jjuuko Murushid na Hassan Isihaka.Owino alikuwa miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha kwanza cha Simba mwanzoni mwa msimu huu timu hiyo ilipokuwa chini ya kocha Patrick Phiri kiasi cha kupewa unahodha. Ujio wa kocha mpya wa timu hiyo Goran

Tambwe aweka rekodi ya kutisha Ligi Kuu

Picha
STRAIKA wa Yanga, raia wa Burundi, Amissi Tambwe, ameweka bonge la rekodi ya kutisha kwa kuwa mchezaji wa kwanza kupiga hat-trick (mabao matatu mechi moja) ya pili msimu huu, ikiwa ni ya nne kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam. Mrundi huyo ni mchezaji pekee aliyeweka rekodi hiyo ambayo haijawahi kuwekwa na mchezaji yeyote tangu uwanja huo ulipoanza kutumika. Mechi ya kwanza kwa straika huyo kufunga hat trick kwenye uwanja huo ilikuwa ni Februari Mosi, 2014, dhidi ya JKT Oljoro, akiwa na Simba, ambayo ilishinda 4-0. Mechi nyingine ambayo Mrundi huyo alifunga hat trick ilikuwa ni Septemba 19, 2014 dhidi ya

Ngassa afichua siri ya ubingwa Jangwani

Picha
WINGA wa kutegemewa wa mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara (Yanga), Mrisho Khalfani Ngassa 'Anko,' amefichua siri ya timu hiyo kutwaa ubingwa msimu huu kuwa ni uwepo wa benchi la ufundi lenye weledi wa soka. Yanga juzi iliweza kutangaza ubingwa baada ya kuifunga Polisi Morogoro mabao 4-1 na kufikisha jumla ya pointi 55, ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote hata mabingwa wa msimu uliopita, Azam FC waliopo nafasi ya pili na pointi 45 katika msimamo wa ligi hiyo. Ngassa ameliambia DIMBA Jumatano kuwa mafanikio ya kikosi chao yanatokana na ujuzi wa makocha wao. Ngassa alisema pongezi nyingi zinastahili kwenda kwa makocha Hans  van der Pluijm  pamoja na msaidizi wake, Charles Mkwassa, ambao wameweza kuwaweka wachezaji kuwa kitu kimoja na hamasa wanazozitoa pindi kikosi kinapopata matokeo mazuri  au mabaya ndizo zilizochangia kujituma kwa kila mmoja wao.

Goran aibadilishia kikosi Azam

Picha
KOCHA Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic, ameamua kubadili kikosi chake ili aweze kuifanyia kitu mbaya Azam FC katika mchezo utakaozikutanisha timu hizo wikiendi hii kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.   Goran Kopunovic Simba na Azam zitapambana Jumapili kuwania kuweka sawa mipango ya kushika nafasi ya pili, ili kupata tiketi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani. Azam wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 45, Simba wakiwa nyuma yao katika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 41, wakibakiwa na michezo miwili, huku wakiwaombea mabaya Wanalambalamba hao wapoteze michezo yao mitatu ili wawapiku. Kama Simba watashinda michezo yao hiyo miwili dhidi ya Azam na JKT Ruvu na Wanalambalamba hao wakafanya vibaya michezo yao, ikiwamo huo wa Simba, Yanga pamoja na Mgambo JKT itawapa fursa ya kumaliza nafasi ya pili. Kutokana na hali hiyo, Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic, ameanza kuzichanga vema karata