Machapisho

Boko Haram wauteka mji muhimu Nigeria

Picha
Wanajeshi wa serikali ya Nigeria. Kundi la Boko haram limefanya mashambulizi katika mji wa Bama na kusababisha mauaji ya watu wengi huku wengine wakitoroka. Wanamgambo hao waliuteka mji wa Bama ,ambao ni wa pili kwa ukubwa katika jimbo la Borno siku ya Jumatatu baada ya jaribio la awali la kutaka kuuteka mji huo kuzimwa na vikosi vya serikali. Akizungumza na BBC ,wakaazi wamethibitisha kuwa mji huo umetekwa na kundi hilo na kwamba maelfu ya watu sasa wameachwa bila makao. Mamlaka ya Nigeria bado haijatoa tamko lolote kuhusu shambulizi hilo. Taarifa zinasema kuwa watu wengi wametoroka wakiwemo wanajeshi. Hapo awali jeshi la Nigeria lilitoa ripoti kuonyesha kuwa mpaka sasa limewaua wapiganaji 70 wa Boko Haram ,kutokana na mapigano kati ya kikundi hicho na wanajeshi Kaskazini -Mashariki mwa mji wa Bama. Boko Haram walifika mapema asubuhi katika mji huo kwa magari ya kivita.Taarifa k...

Mwandishi mwingine "achinjwa"

Picha
Mwandishi aliyechinjwa na IS Steven Sotloff Wapiganaji wa dola ya Kiislam IS wamesambaza picha za video katika mitandao kwa lengo la kuonyesha kuchinjwa kwa mwandishi wa habari raia Marekani Steven Sotloff ambaye ni mmoja wa mateka wanaoshikiliwa na wapiganaji hao. Mwandishi huyo Sotloff, mwenye umri wa miaka 31 ambaye alitekwa na wapiganaji hao mwezi August mwakajana. Mwezi uliopita Sotloff alionekana mwishoni katika picha za video zilizoonyeshwa kuhusiana na kuchinjwa kwa mwandishi mwingine wa Marekani James Foley. Wapiganaji hao wa katika picha hizo pia wameonekana wakimtishia kumuua mateka mwingine anayedhaniwa kuwa ni raia wa Uingereza. Baada ya mauaji ya mwandishi wa awali Foley, mama mzazi wa mwandiashi wa Sotloff alitoa ombi maalumu kwa kiongozi wa wanajeshi hao Abu Bakr al-Baghdadi kutoa muua mtoto wake. Msemaji wa Ikulu ya White House Josh Earnest amesema kuwa maofisa wa Ma...

Kiongozi wa Al Shabaab ashambuliwa

Picha
Haijulikani ikiwa Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo Wanajeshi wa Mreakani wamefanya mashambulizi ya angani dhidi ya msafara wa magari ya mmoja wa viongozi wa kundi la Al Shabaab nchini Somalia. Haijulikani ikiwa kiongozi wa kundi hilo, Ahmed Abdi Godane aliuawa kwenye shambulizi hilo lililofanyika umbali wa kilomita 240 kusini ya mjini mkuu Mogadishu. Mwandishi wa BBC anasema kuwa wanajeshi wa Marekani walionekana wakishuka katika eneo hilo kwa helikopta na kuchukua miili ya wapiganaji waliouawa. Msemaji wa idara ya ulinzi ya Marekani, (Rear Admiral John Kirby) alisema bado inadurusu matokeo ya shambulizi hilo. Baadhi ya taarifa zinasema kuwa wapiganaji waliwakamata wakazi walioshukiwa kutoa taarifa kwa Marekani.-bbc

Ni gari la polisi au Rais lililoibiwa Kenya?

Picha
Msemaji wa serikali amekanusha madai kuwa gari lililoibiwa lilikuwa la ulinzi wa Rais  aarifa za kutatanisha za kuibiwa kwa gari la ulinzi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta zimeibuka nchini humo. Taarifa hii ilitolewa na baadhi ya vyombo vya habari ingawa msemaji wa Rais Kenyatta ameikanusha taarifa hiyo akisema kuwa gari lililoibiwa lilikuwa la idara ya polisi likiendeshwa na inspekta mkuu wa polisi. Gari hilo lililokuwa lisemekana kuwa na uwezo wa kuhimili risasi, liliibiwa usiku wa Jumatano na kwamba aliyekuwa analiendesha gari hilo alikuwa afisa wa polisi. Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye mtandao wa Daily Nation ikimnukuu mtu anayesemekana kuwa dereva wa gari hilo la kifahari alilazimishwa kuvua nguo zake kabla ya kupokonywa gari hillo. Gari lenyewe lilikuwa na nambari ya usajili ya kibinafsi. Ni gari la polisi au la Rais? ...

Mrembo apokonywa taji kwa ujeuri wake Burma

Picha
May Myat Noe Mshindi wa mashindano ya taji la Miss Asia Pacific World, May Myat Noe, amevuliwa taji lake akisemekana ni mjeuri, hana hadhi na hastaili taji hilo. May Myat Nwoe alivishwa taji lake mwezi Mei baada ya kufanyiwa upasuaji na kuwekwa matiti bandia kufuatia ombi la waandalizi wa mashindano hayo wa Korea. Baadaye walimlaumu wakisema hataki kushirikiana nao na sasa wanataka aombe radhi na pia arejeshe taji alilovishwa. Waandalizi walisema hawajafurahishwa na kitendo cha msichana huyo kumpeleka mamake nchini Korea Kusini. May Myat Noe, mshindi wa kwanza wa tuzo hiyo kutoka Burma, sasa anaripotiwa kutoweka na taji alilovikwa aliposhinda mwaka jana. Msemaji wa waliodhamini taji hilo anasema msichana huyo wa miaka 18 alitoweka baada ya kufahamishwa uamuzi huo wa kumpokonya taji hilo wiki jana. BBC imefahamishwa kwamba waa...

Balozi wa Guinea amjeruhi mwanawe

Picha
Polisi wa jiji la Washington Polisi nchini Marekani wameshindwa kumkamata balozi wa Equatorial Guine mjini Washngton, kwa tuhuma za kumpiga binti yake kwa mguu wa kiti cha mbao, balozi huyo hajakamatwa mpaka sasa kutokana na kinga yake ya kibalozi alonayo . Msemaji wa polisi Dustin Sternbeck amesema kwamba walipewa taarifa mapema wiki hii kua kuna tukio nyumbani kwa balozi huyo, na walipofika wakamkuta binti huyo mdogo akiwa na jeraha kubwa kichwani mwake ambaye alihitaji tiba na hivyo kumpeleka hospitalini kwa matibabu. Pamoja na hayo yote Dustin alisema kua polisi hawana mamlaka kwa kesi za namna hiyo zinazowahusisha wanadiplomasia lakini wamekwisha iarifu serikali juu ya suala hilo.

NATO yaonyesha picha za askari wa Urusi

Picha
Picha za Nato za satelaiti zikiwaonyesha askari wa Urusi ndani ya ardhi ya Ukraine Umoja wa kujihami wa nchi za Magharibi, Nato wametoa picha za satelaiti zinazowaonyesha askari wa Urusi wakiwa na silaha ndani ya nchi ya Ukraine kuwasaidia waasi wanaotaka kujitenga kupambana na majeshi ya serikali ya Ukraine. Rais wa Ukraine amefanya mkutano wa baraza la usalama Alhamisi kuhusu hali iliyopo nchini humo. Urusi imekana madai hayo. Mapema, waasi waliteka mji wa pwani ya Novoazovsk ulioko kusini. Watu wapatao 2,119 wameuawa katika mapigano yaliyodumu kwa miezi minne. Rais Barack Obama wa Marekani Rais Barack Obama amesema Urusi inahusika na ghasia za mashariki mwa Ukraine. Katika taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Marekani, Bwana Obama amesema waasi katika eneo hilo wamepatiwa mafunzo, silaha na kufadhiliwa na Urusi. Hata hivyo, kauli ya Bwana Obama imekuwa na mashaka aliposema Mareka...