Afrika inaongoza kwa magonjwa

ASILIMIA 25 ya magonjwa wanaougua binadamu hapa duniani yanapatikana katika bara la Afrika.

Hayo yamebainishwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Seif Suleiman Rashid katika mkutano wa Madaktari Bingwa wa Upasuaji (TSA).

Dk. Seif Suleiman Rashid amesema kuwa kutokana na wingi wa maradhi kuliandama bara hilo imekuwa sababu kubwa ya kuwepo kwa hitaji la madaktari zaidi.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi87lS0wgGV4IpwPRvfavBIeET6JMNuJhrUJN-QfM2MoI9nZ0K3mVihtCoEwaSgmWCw__oGKSHVzTPW6A80D5lIfVtrZuNdWSMNBYJroTiljpy0ZsQEkZQkdu_tiZm4DBEpUUqpqxNMfvSy/s1600/A.JPG

DK. Rashid amesema kuwa pamoja na Afrika kukumbwa na maradhi zaidi lakini hadi sasa ina asilimia tatu ya madaktari bingwa hususan katika fani ya upasuaji ambao hawakidhi mahitaji halisi ya kutoa huduma hiyo.

‘Bado tuna safari ndefu sana ya kukabiliana na upungufu huu wa madaktari bingwa katika fani ya upasuaji ambayo ni muhimu katika maisha yetu,”.

Waziri amekimwagia sifa Chama cha Madaktari bingwa wa upasuaji (TSA) kwa juhudi wanazozifanya kupambana na tatizo la upungufu wa madaktari bingwa.

Amesema kuwa ili kuhakikisha kunapatikana ongezeko la madaktari bingwa, serikali imekuwa karibu na chuo cha madaktari bingwa kilichopo Arusha kinachotoa elimu ya juu katika fani ya upasuaji kwa kuwapa misaada ya hali na mali.

Akizungumzia changamoto zinazolikabili bara la Afrika katika fani ya utabibu amesema ni pamoja na kutokuwepo kwa miundo mbinu, vitendea kazi pamoja na rasilimali watu.

“Tunahitaji kuwekeza nguvu nyingi kuweza kufikia malengo ya milenia kama kweli tunahitaji kufanikiwa katika hili lazima tuweke nguvu ya pamoja kati ya Wananchi na serikali,”.

Katika mkutano huo Dk. Rashid alitoa vyeti kwa madaktari bingwa wa upasuaji 61 toka katika chuo cha kitabibu kilichopo Arusha pamoja na vyeti kwa madaktari bingwa wastaafu katika fani ya upasuaji ambao ni Profesa Philemon Sarungi, Profesa Joseph Shija na Profesa Cray Bernard.

Kwa upande wake Rais wa TSA, Paul Marealle amesema kuwa sekta ya afya hapa nchini bado inahitaji nguvu ya ziada kuiweka sawa.

Amesema kuwa vifo vingi vya akina mama na watoto hususani katika maeneo mengi hapa nchini ni matokeo ya nchi kushindwa kuwekeza inavyotakiwa katika sekta hiyo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4