Machapisho

Yanga yapata ulaini Tunisia

Picha
YANGA imepata mteremko kuelekea mchezo wao wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Etoile ya Tunisia, kwani imepata mbinu zitakazowawezesha kuwashika pabaya wapinzani wao hao. Mchezo huo ni wa raundi ya pili ya michuano hiyo ambapo katika mchezo wa kwanza uliopigwa Jumamosi iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Matokeo hayo yanaipa kibarua kigumu Yanga mjini Tunis kwani watalazimika kushinda au kupata sare ya zaidi ya mabao 2-2 ili iweze kusonga mbele na kutinga hatua ya mtoano kuwania tiketi ya makundi. Kwa kufahamu ugumu wa mchezo wa marudiano, Yanga imepanga kufanya kila mbinu wanazoweza ili kuwajengea mazingira mazuri ya kushinda na kuwatoa Etoile. Miongoni mwa mbinu hizo ni kuwahi mapema nchini Tunisia ili kuzoea hali ya hewa ya huko ambayo ni ya baridi na kukutana na Watanzania waishio huko ili waweze kuwapa mikakati ambayo wanaweza kuitumia kukwepa hila za wapinzani wao hao na kushinda. ...

Simba yaipumlia Azam

Picha
KLABU ya soka ya Simba imeendeleza kampeni zake za kuwania nafasi ya pili katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya jana kuishindilia Mgambo JKT mabao 4-0, huku mshambuliaji wake hatari, Emmanuel Okwi, akiondoka na mpira kwa kupachika wavuni mabao matatu. Mchezo huo wa marudiano umepigwa kwanye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo, ambapo  Simba walikuwa wamepania kulipiza kisasi cha kufungwa mabao 2-0 katika mchezo wa awali uliopigwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Matokeo ya ushindi wa leo yameiwezesha Simba kufikisha pointi 38 na kuongeza ushindani wa kuchuana vikali na mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Azam FC, kukata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani. Simba na Azam wametofautiana kwa pointi nne tu, ambapo Azam wanashika nafasi ya pili wakiwa na pointi 42 baada ya kushuka dimbani mara 22, huku wapinzani wao wakiwazidi kwa mchezo mmoja. Okwi aliandika bao la kuongoza kwa Simba dakika ya nane, akiunganisha pasi safi ya Hassan Ramadhani K...

Mabeki Yanga wamchefua Pluijm

Picha
KOCHA Mkuu wa Yanga Mholanzi, Hans van Der Pluijm, ameelezea kukerwa na uzembe uliofanywa na mabeki wake wa kuruhusu kufungwa kirahisi, huku akionyesha hali ya ukali kwa kila mchezaji aliyeshindwa kutimiza majukumu yake ipasavyo. Pamoja na makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa juzi wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Stand United. Akizungumza jijini Dar es Salaam , Pluijm alikiri kuwa kikosi chake kilikuwa na bahati ya ushindi katika mchezo huo licha ya upinzani mkali walioupata kutoka kwa wachezaji wa Stand ambao walicheza kwa kiwango cha juu. Alisema kiungo Simon Msuva na mshambuliaji Amissi Tambwe walikosa nafasi za wazi, ambazo zingeweza kuongeza idadi ya mabao huku akidai soka ni mchezo wa makosa siku zote hivyo lolote linaweza kutokea. Pluijm aliendelea kusisitiza kwamba, mawasiliano ni kitu muhimu kwa wachezaji wanapokuwa uwanjani, huku akiwashushia lawama wale walioonekana kufany...

Nyota wa ligi ya NBA kukipiga Afrika

Picha
Luol Deng Chama cha Mpira wa Kikapu cha Marekani, NBA kimetangaza Jumatano mipango ya kucheza mchezo wake wa kwanza barani Afrika, katika mchezo wa mwezi Agosti ambao utawashirikisha wachezaji wa mpira wa kikapu barani Afrika katika jitihada za kuufanya mchezo huo kupata mashabiki duniani. Mechi ya Agosti Mosi mjini Johannesburg itaundwa na timu ya Afrika "Team Africa" ikiwashirikisha wachezaji nyota wa mpira wa kikapu wa ligi ya NBA wa kizazi cha kwanza na cha pili kutoka Afrika dhidi ya timu ya dunia"Team World,"ambayo itakuwa na wachezaji kutoka maneo mengine duniani. Mchezaji nyota mara mbili wa NBA All-Star, Luol Deng wa timu ya Miami Heat, ambaye alizaliwa katika nchi ambayo kwa sasa ni Sudan Kusini, ataongoza timu ya Team Africa, wakati nyota mara nane wa NBA Chris Paul wa Los Angeles Clippers atakuwa nahodha wa timu ya Team World. Tangazo hilo limetolewa wakati ligi ya Marekani imetangaza kalenda yake ya mwaka kwa michezo ya nje...

Wafuasi wa dhehebu wauawa Angola

Picha
Angola Wanachama kadha wa dhebu moja lililojihami wameuawa kwenye mapigano na vikosi vya usalama nchini Angola. Chama kikuu cha upinzani nchini humo cha UNITA kilisema kuwa huenda watu 200 waliuawa huku chama tawala cha MPLA kikisema kuwa ni watu 13 waliuawa. UNITA kinaitaka serikali ya Angola kuchunguza vifo vya waumini wa dhebu la Seventh Day Light of the World ambalo lilijitenga kutoka kanisa la Seventh Day Adventist. Dhehebu hilo linamini kuwa dunia itaisha mwishoni mwa mwaka huu na limetoa witu kwa wafuasi wake kuondoka makwao na kuelekea milimani. bbc

Mashambulizi yaanza tena Yemen

Picha
Ndege ya Saudi Arabia yaenda kushambulia Yemen Muungano unaongozwa na Saudi Arabia umerejelea tena mashambulizi ya angani dhidi ya waasi wa Houthi nchini Yemen huku pia kukiendelea mapigano ya ardhini. Kuanza tena kwa mashambulizi hayo kunakuja saa kadhaa baada ya Saudi Arabia kutangaza kuwa mashambulizi hayo yamefanikiwa na kwamba yalikuwa yanafika mwisho. Mashambulizi hayo yalianza baada ya waasi kuteka makao makuu ya jeshi kwenye mji wa Taez. Licha ya hili habari zinasema kuwa makubaliano yanatarajiwa kuwepo na waasi hao.

Siku tatu za maombolezo Ethiopia zaanza

Picha
Islamic State wakienda kuwaua raia wa Ethiopia Ethiopia imeanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa heshima za raia wake waliouawa na wanamgambo wa kundi la Islamic State nchini Libya. Bendera zitapepea nusu mlingoti wakati nalo bunge la nchi hiyo likikutana kujadili hatua ambazo litachukua kufuatia mauaji hayo ya raia wake zaidi ya ishirini. Msemaji wa serikali Redwan Hussein, alisema kuwa waathiriwa hao wanaaminika kuwa wahamiaji waliojaribu kusafiri kwenda barani ulaya. Mungano wa Afrika ambao una makao yake makuu nchini Ethiopia ulilaani mauaji hayo na kusema kuwa utafanya mikakati ya kuhakikisha kuwepo usalama nchini Libya. Wanamgambo wa Islamic State walitoa kanda ya video ambayo inakisiwa kuonyesha mauaji hayo yanayoonyesha watu hao wakipigwa risasi na kukatwa vichwa.