Okwi: akili kubebwa J’mosi
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Simba, Emmanuel Okwi, amemshukuru mwamuzi wa mchezo wao dhidi ya Mtibwa Sugar uliochezwa Jumamosi iliyopita, Abdallah Kambuzi wa Shinyanga, kwa kuongeza dakika tano baada ya dakika 90 za muda wa kawaida, hivyo kuwawezesha kufunga bao pekee lililoipa timu yake ushindi wa 1-0. Okwi alifunga bao hilo dakika ya tatu kati ya tano za muda wa nyongeza, wakati timu hizo zikiwa hazijafungana katika mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mganda huyo alifunga bao hilo kwa staili ya aina yake, akipiga shuti kali akiwa umbali wa mita 25 kutoka lango la Mtibwa baada ya kupokea pasi kutoka kwa Abdi Banda. Kabla ya kufunga bao hilo wakati baadhi ya mashabiki wakiwa wametoka uwanjani wakijua matokeo ni suluhu, aliwahadaa mabeki na kumchungulia kipa wa wapinzani wao hao alivyokaa na kupiga mpira mrefu uliokwenda moja kwa moja wavuni. Okwi alisema miongoni mwa watu anaowashukuru kwa kumpa nguvu ya kutafuta bao ni mwamuzi huyo, b...