TRA kutoa elimu,sheria ya kodi

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imesema inajipanga kutoa elimu ya ulipaji kodi na sheria za kodi kwa wajasiliamali pamoja na wafanyabiashara wengine kutoka nje ya nchi ili waweze kutambua umuhimu wake.http://www.ippmedia.com/media/picture/large/trataxenvngos(8)(3)(9)(3).jpg
Afisa Mkuu katika Idara ya Huduma na Elimu kwa Walipa Kodi (TRA), Yeremiah Mbaghi, alisema kila mwaka wamekuwa na kawaida ya kukutana na wafanyabiashara kutoka China kwa lengo la kuwaelimisha masuala ya ukusanyaji kodi pamoja na sheria za kodi kutokana na kuwa sheria za nchi hizo mbili zinatofautiana.
Mbaghi aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa semina ya elimu ya kodi iliyowashirikisha  wafanyabiashara na wawekezaji kutoka  China.
 “Tutakuwa tunatoa elimu ya kodi kwa wajasiliamali mbalimbali wa ndani, wafanyabiashara wa  nje pamoja na wawekezaji lakini leo ni zamu ya wachina na tutakuwa tunatoa kwa siku maalumu kwa kila sekta tofauti,” alisema Mbaghi.
Naye Mshauri wa Kisiasa katika Ubalozi wa China, Li Xuhang, amewataka wafanyabiasha na wawekezaji kutoka China kuhudhuria semina za elimu ya ulipaji kodi zinazotolewa na TRA kwa lengo la kujifunza.
Aidha aliwataka kulipa kodi kwa hiyari pamoja na kufuata sheria zake.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4