Simba yaipumlia Azam

KLABU ya soka ya Simba imeendeleza kampeni zake za kuwania nafasi ya pili katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya jana kuishindilia Mgambo JKT mabao 4-0, huku mshambuliaji wake hatari, Emmanuel Okwi, akiondoka na mpira kwa kupachika wavuni mabao matatu.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRwoWjZxRRk5s9-7hHvBLqvL6GWz2ngTh_cbom1tPtrOeKV0N-H0RpkUXrcQtUPI9dhZQ8Hf8mUcKVmcLoatX9tPNO4gVfCL85FLCcG3wn_ZR-mtJSj7mISPv0z81eh9W9UFH3oGAwi1g/s1600/SIMBAGPL.JPG
Mchezo huo wa marudiano umepigwa kwanye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo, ambapo  Simba walikuwa wamepania kulipiza kisasi cha kufungwa mabao 2-0 katika mchezo wa awali uliopigwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Matokeo ya ushindi wa leo yameiwezesha Simba kufikisha pointi 38 na kuongeza ushindani wa kuchuana vikali na mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Azam FC, kukata tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.
Simba na Azam wametofautiana kwa pointi nne tu, ambapo Azam wanashika nafasi ya pili wakiwa na pointi 42 baada ya kushuka dimbani mara 22, huku wapinzani wao wakiwazidi kwa mchezo mmoja.
Okwi aliandika bao la kuongoza kwa Simba dakika ya nane, akiunganisha pasi safi ya Hassan Ramadhani Kessy na kuachia shuti lililotinga moja kwa moja wavuni.
Simba nusura wapachike wavuni bao la pili dakika ya 10 kupitia kwa Okwi tena, lakini shuti lake lilitoka nje ya lango huku kipa wa Mgambo JKT, Godson Mmasa akiwa tayari ametoka golini kwake.
Kiungo mshambuliaji Ramadhani Singano ‘Messi’, ambaye alipiga mpira wa adhabu ndogo aliwaamsha mashabiki wa Simba  dakika ya 25, baada ya kupiga shuti lililogonga mwamba na kutinga wavuni na kumuacha kipa wa Mgambo akishangaa asijue cha kufanya.
Dakika ya 40 Okwi alifunga bao la tatu, baada ya kuwatoka mabeki wa Mgambo ambao walishindwa kumkaba na kuwapiga chenga, kabla ya kuachia shuti lililotinga moja kwa moja wavuni.
Salum Gila wa Mgambo alijaribu bahati yake kutaka kuiandikia bao timu yake dakika ya 43, lakini shuti lake lilipaa juu na kutoka nje, hivyo kuifanya Simba kwenda mapumziko wakiongoza kwa mabao 3-0.
Katika mchezo mwingine wa ligi  uliochezwa kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, wenyeji Polisi Morogoro walitoka suluhu na Coastal Union na kuzidi kujiweka katika mazingira mabaya ya kushuka daraja msimu huu.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4