North Mara yaibuka kidedea

KAMPUNI ya madini ya North Mara Gold Mine imeibuka mshindi wa jumla wa Tuzo za Rais za Huduma za Jamii na Uwezeshaji (CSRE), zilizotolewa kwa Makampuni yaliyofanya vizuri kwenye ushiriki wa miradi ya kijamii wa mwaka 2014.
http://www.ulsprojects.com/wp-content/uploads/2012/07/North_Mara.jpg
Kampuni hiyo pia imefanikiwa kushinda tuzo ya jumla ya Kampuni kubwa ya Madini baada ya kuonekana kuchangia zaidi miradi mbalimbali katika sekta za elimu, afya, miundombinu na ajira.
Akizungumzia wakati akikabidhi tuzo hizo jijini Dar es Salaam , Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal amesema tuzo hizo zina lengo la kuwahamasisha wawekezaji kurejesha shukrani kwa jamii inayozunguka migodi hiyo.
Bilal alisema kuwa kila mwaka shindano hilo limekuwa likiboreshwa hali iliyochangia kuvutia kampuni nyingi kushiriki tofauti na mashindano ya mwaka jana ambapo kampuni zilizoshiriki zilikuwa 38 lakini mwaka huu idadi imeongezeka na kufikia 59. 
Naye Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene akizungumzia tuzo hizo amesema serikali imedhamiria kuwawezesha wawekezaji wa Madini kuwafaidisha wananchi wa maeneo wanayoishi kwa kuwaajiri au kununua bidhaa zao.
“Wananchi wanaokuwa wanazunguka migodi hiyo wanahitaji kuona wanajengewa barabara nzuri, wanajengewa hospitali nzuri, wanafunzi wanapata madawati, shule nzuri, kwani hivyo ni vitu vya msingi kufanyika hivi sasa.
“Kwa sasa tumefikia wakati wa kuwawekea sheria na taratibu ambazo zitawasaidia kujua vigezo vinavyohitajika kupata ushindi,” amesema.
Kampuni nyingine zilizopata Tuzo ya Kampuni ndogo za Madini (Busolwa Mining Limited), Kampuni ya uzalishaji wa mafuta na gesi (Songas), Kampuni ya utafutaji wa mafuta na gesi (Afren Tanzania).
Tuzo nyingine ya Utafutaji wa Madini (Mantra Tanzania Limited), Tuzo ya Kampuni ya kati ya Madini (Shanta Mining (T) Limited), Kampuni kubwa ya Madini (North Mara Gold Mine).
Tuzo nyingine maalumu zilizotolea ni msaada wa Sekta ya Elimu ya Sekondari (Geita Gold Mine Limited), Elimu ya Juu (Statoil Tanzania) na Miundombinu (Buzwagi Gold Mine)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4