Majambazi yaua wafanyakazi Bonite

WATU wawili wamefariki dunia mjini Moshi mkoani  Kilimanjaro, baada ya kupigwa risasi na watu wanaodaiwa kuwa  majambazi.
Wakati wa tukio hilo, majambazi hao walipora mamilioni ya fedha, mali ya Kampuni ya Bonite ya mjini Moshi.http://www.moshi.esthersumner.com/wp-content/uploads/2013/08/IMG_4302_cc.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makunga alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema lilitokea juzi saa 12 jioni katika eneo la Kili FM Soweto.
Kwa mujibu wa mkuu huyo wa wilaya, tukio hilo lilitokea wakati watu hao wawili walipokuwa wakirudi ofisini kutoka kwenye mauzo mitaani.
“Wafanyakazi  wa Bonite walikuwa wakitoka kukusanya mauzo ya kampuni hiyo katika kituo cha Himo, stendi ya mabasi Moshi, Kiusa na Kiboriloni.
“Wakati huo, walikuwa kwenye gari aina ya hiace lenye namba za usajili T 803 ATR na walipofika eneo la Soweto, walivamiwa na majambazi hao,” alisema Makunga.
Alisema  majambazi hao, walikuwa wanne na kwamba wakati wanawavamia wafanyakazi hao walikuwa wamepanda pikipiki mbili.
“Pia, majambazi hao walikuwa na bastola na walipolifikia gari la wafanyakazi wa Bonite, walilivamia na kuanza kumimina risasi na kumpiga mlinzi wa kampuni hiyo kichwani na kufariki papo hapo pamoja na dereva ambaye naye alifariki baada ya kupigwa risasi kifuani.
“Baadaye, majambazi walipora fedha walizokuwanazo na kutokomea kusikojulikana,” alisema.
Aliwataja marehemu hao, kuwa ni mlinzi Edson Shamba, (56), aliyekuwa na bunduki aina ya Shortgun yenye namba 8710653.
Mwingine ni Amin Mselem, (61), mkazi wa Mtaa wa Chunya, Manispaa ya Moshi.
“Pamoja na hayo, maofisa mauzo wa kampuni hiyo waliokuwa kwenye gari hilo hawakujeruhiwa na wanashikiliwa na polisi kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.
“Kutokana na tukio hilo, vyombo vya ulinzi tayari vimeshaanza uchunguzi wa kina na tunawaomba wananchi watoe ushirikiano ili wahusika waweze kukamatwa haraka,” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Geofrey Kamwela, alikiri kutokea kwa tukio hilo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4