HONDA yawatia matatani

WAKAZI wawili Jijini Dar es Salaam, Gift Norah (26) na Hassan Abeid (20) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni  wakikabiliwa na shtaka la kuiba pikipiki yenye thamani ya Sh milioni 2.3
Mbele ya Hakimu Caroline Kiliwa, Wakili wa Serikali Zawadi Mdegela, amedai kwamba tukio hilo lilitokea Machi 17 mwaka huu eneo la Mbezi Beach Wilayani hapo.http://lbjatty.homestead.com/gavel.jpeg
Zawadi aliongeza kuwa watuhumiwa hao waliiba pikipiki yenye namba za usajili T. 818 CQH HONDA inayomilikiwa na Joseph Njuu.
Watuhumiwa baada ya kusomewa shtaka hilo wamekana kosa hilo na upelelezi bado unaendelea ambapo Hakimu Kiliwa alisema dhamana kwa watuhumiwa iko wazi kisheria hivyo aliwataka waje na wadhamini wawili walioajiriwa serikalini ama katika taasisi yoyote inayotambulika kisheria.
Shauri hilo limeahirishwa hadi Mei 6 mwaka huu na watuhumiwa walirudishwa mahabusu kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4