Covenant Benki yaipiga tafu Namtumbo

BENKI ya Covenant ya jijini Dar es salaam imetoa msaada wa saruji yenye thamani ya Sh milioni 2.5 kwa ajili ya umaliaziaji wa ujenzi wa maabara katika Shule ya Sekondari ya Msindo wilayani Namtumbo mkoani Ruvuma.http://api.ning.com/files/3I-9LvQkoOSALvvAIX*2pX-dNeX1bJbsHENYz3BDi68FHt0EM*FNegVeKx*MUA5JXhtgo5FXibk9mZPzwFNBj4HIQK1QfsNg/002COVENANT.JPG
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mkuu wa benki hiyo, Sabetha Mwambeja alisema msaada huo ni utekelezaji wa sera yao ya kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwa jamii.
Amesema Conenant benki ina program za kusaidia shughuli za kijamii hususani katika sekta zisizokuwa rasmi pamoja na vijana kwa kuwezesha upatikanaji na uwezeshaji wa masomo kwa njia moja au nyingine.
Naye Mjumbe wa Bodi ya benki hiyo, Margareth Kyarwenda amesema benki inatambua masomo ya sayansi ni muhimu katika nchi na maabara ni sehemu ya maandalizi ya wataalam wa fani hiyo.
“Tunatambua BRN (Mpango wa Matokeo Makubwa sasa) kwa kiasi kikubwa inategemea sayansi na teknolojia hivyo benki ipo mstari wa mbele kuhakikisha nchi inasomesha na inakuwa na wataalam wa kutosha kupitia shule hizi” amesema Margareth.
Akipokea msaada huo, Diwani wa Kata ya Msindo, Mohammed Birika amesema mchango huo niwa pili kwa shuele hiyo ambapo awali benki hiyo ilisaidia ujenzi wa vyumba vya madarasa pamoja na ofisi ya utawala katika shule hiyo.
“Tunashukuru msaada wa benki hii kwani umechangia kwa kiasi kikubwa ufaulu wa wanafunzi katika shule yetu ya Msindo ambapo kila mwaka wanafunzi wanafaulu na kuendelea kidato cha sita katika sehemu mbalimbali nchini”amesema Birika

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4