Anna Kilango ajipigia debe

MBUNGE wa Same Mashariki ambaye pia ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Anna Kilango Malechela, amesema anawacheka watu wanaopita jimboni kwake na kutangaza kuwania ubunge katika jimbo hilo.http://www.thecitizen.co.tz/image/view/-/1851672/lowRes/511868/-/hmqdhw/-/kilango.jpg
Kilango alitumia fursa ya ziara yake ya mara ya kwanza katika Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kujipigia debe ambapo alisema kujituma kwake na kufanya kazi aliyotumwa na wananchi vizuri ndiko kunakompa kujiamini kuwa atachaguliwa tena.
Kilango alitoa kauli hiyo jana wakati akizungumza na wafanyakazi wa Mamlaka hiyo hivi karbuni ambapo aliwaasa kufanya kazi kwa kujituma kwani ndio msingi wa mafanikio ukiachilia mbali changamoto zilizopo.
“Mtu anayefanya kazi vizuri anakuwa na amani na hana wasiwasi. Hata mimi najua kuna watu wanajipitisha huko jimboni wanataka ubunge lakini mimi nawacheka tu kwa sababu sina wasiwasi na wala siwezi kujibizana nao. Ikifika hiyo siku ya kujinadi nitawaeleza wananchi nilichofanya na naamini watanichagua tena kwa sababu nimefanya kazi nzuri,” alisema Kilango.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya TEA Naomi Katunzi alisema Mamlaka hiyo inachangamoto ya uhaba wa rasilimali fedha kwakuwa mahitaji ya taasisi za elimu ni mengi na hivyo kuwataka wadau na wananchi kuchangia elimu kupitia mfuko wa elimu uliopo chini ya mamlaka hiyo.
“Tunaomba watanzania wawe na moyo wakuchangia elimu kama wanavyochangia kwenye harusi na sherehe zingine,” alisema Katunzi na kuongeza, “kwa sasa tunapokea fedha kidogo sana kutoka kwa wadau wakiwemo wananchi lakini bado tunawahamasisha waendelee kujitoa kama wenzetu wa mataifa ya magharibi wanavyofanya na ndio maana wameendelea sana kielimu.”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4