Yanga yawashika pabaya simba kwa okwi

MSHAMBULIAJI hatari wa Simba, Emmanuel Okwi, amefichwa katika moja ya hoteli za kifahari jijini Dar es Salaam, huku Yanga wakitajwa kuhusika na hatua hiyo.
Tukio hilo limekuja zikiwa ni siku chache kabla ya Simba kuvaana na Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Jumapili hii.
Sababu za Yanga kuhusika na kufichwa kwa Okwi, zinatokana na undugu baina yao, kwani alishawahi kufanya kazi Jangwani, lakini pia akitajwa kuwa na uhusiano mzuri na baadhi ya wanachama na matajiri wa klabu hiyo.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimtwnKmTN_MnUpbaxbe91IqUhkr5GfrvcoyFCC3p8rc1YjzK8-pNQV6ivJoEGgsf-1N5CMAJ1tpU6zRf_zvinraa6PdzokFON_c3_Vma-rzi6jlV4rg4IHLZYsAftFZPVtRaIMqPtnYSI/s1600/_HMB7076.JPG
Ni kutokana na kufahamu hilo, uongozi wa Simba juzi ulifanya uamuzi wa ghafla kwa kuwapeleka katika hoteli maalumu Okwi na wachezaji wenzake wa Uganda, Danny Sserunkuma na Jjuuko Murushid, ili kuvuruga mawasiliano yoyote yanayoweza kufanywa baina ya Yanga na Okwi.
Uongozi wa Simba unafahamu kuwa iwapo Yanga watapata fursa ya kukutana na Okwi, wanaweza kumrubuni ili kucheza chini ya kiwango au kuwasaidia kwa njia yoyote ile kuepuka kipigo siku hiyo.
Mmoja wa kiongozi kutoka ndani ya klabu hiyo, alilipasha BINGWA kuwa uamuzi wa kuwaficha wachezaji hao umekuja mara baada ya kumalizika kwa mechi yao dhidi ya Tanzania Prisons.
“Tunajua fitna za wapinzani wetu, Yanga, ndio sababu ya kuamua uamuzi huu wa kuwaweka wachezaji hao kwenye hoteli ya pamoja ili kuepuka hujuma,” alisema.
Chanzo hicho kilisema kikosi cha timu hiyo kimeondoka asubuhi kuelekea Zanzibar kwa ajili ya kambi ya kusubiri mechi hiyo inayosubiriwa na mashabiki mbalimbali.
BINGWA lilimtafuta Katibu wa Simba, Stephano Ali kuzungumzia kambi hiyo ya Zanzibar na kusema kikosi hicho kimeondoka na wachezaji wote, kasoro Simon Sserunkuma aliyekuwa nchini Uganda kwa matatizo ya kifamilia.
Alisema kikosi hicho kimeondoka na Kocha Msaidizi, Suleimani Matola, huku kocha mkuu, Kopunovic akiomba kupumzika kwa siku mbili jijini Dar es Salaam kabla ya kuungana na wachezaji wake.
“Timu imeondoka saa 6:00 wakati mkutano mkuu ukiendelea na imeondoka na Matola, huku Kocha Mkuu akitarajiwa kuungana na timu yake keshokutwa,” alisema.
Simba inashika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 24, baada ya kushuka dimbani mara 16, wakati Yanga wakiwa kileleni na pointi zao 31 kutokana na mechi 15.-bingwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4