Pluijm aibua mapya Yanga

KOCHA Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm, ameutaka uongozi wa klabu hiyo kusaka mikanda ya video za wapinzani wao wajao katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, FC Platnum ya Zimbabwe.
Yanga Ijumaa iliyopita ilitinga raundi ya kwanza ya michuano hiyo baada ya kuitoa BDF XI ya Botswana katika raundi ya awali kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2.http://api.ning.com/files/qB*eEYpVu7NddqdvVkVHx-dEcToHd*l9wI8uWULRac-eoJK21BYyRSETIj6Z8pNn8ip4Lsru7vO3bIPDRl05jTGtAwkNAV7b/PLUIJMKITAMBI.jpg?width=650
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga walishinda mabao 2-0 kabla ya kulala kwa mabao 2-1 ugenini Ijumaa iliyopita.
Katika raundi inayofuata, Yanga watakutana na FC Platnum iliyoitoa Sofapaka ya Kenya.
Kwa kufahamu ugumu wa mchezo huo, Pluijm ameanza kujipanga mapema kuhakikisha anawatoa Wazimbabwe hao na kusonga mbele, hicho kikiwa ndicho kipaumbele chake, kuhakikisha Yanga inafanya kweli katika soka la kimataifa.
Akizungumza na BINGWA jana kabla ya safari ya kurejea nchini Tanzania, Pluijm alisema akipata mikanda ya kama 10 ya wapinzani wake wajao, hatakuwa na sababu ya kushindwa kuwatoa kwenye michuano hiyo.
“Nataka kuwasoma zaidi kuona ni vipi ninaweza kuwaandaa wachezaji wangu kupambana nao, sina wasiwasi na timu yangu, kwa sasa imeiva na mchezo wetu wa juzi (Ijumaa) wa ugenini, umetusaidia sana kwani wachezaji wangu wamejifunza mambo mengi, ikiwamo kukabiliana na wapinzani ugenini,” alisema Mholanzi huyo.
Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kutua nchini leo kutoka Botswana na kwamba baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, kitakwenda moja kwa moja Bagamoyo kujichimbia kuiwinda Simba katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara utakaopigwa wikiendi hii.
Mchezo huo dhidi ya Simba unatarajiwa kuwa na msisimkoa wa aina yake kwani timu zote mbili zimeonekana kupania kutoka uwanjani na ushindi.
Kwa upande wao, Simba walitarajiwa kuondoka Dar es Salaam jana kwenda kuweka kambi Zanzibar, kama sehemu ya maandalizi ya kuwaangamiza Yanga.
Katika mzimamo wa ligi hiyo, Yanga wapo kileleni na pointi zao 31, wakati Simba inashika nafasi ya tatu kwa pointi 24, ikiwa imecheza mechi moja zaidi ya watani wao hao wa jadi. -bingwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4