Goran: Wembe ni ule ule Tanga


BAADA ya kuibuka na ushindi mara tatu mfululizo, Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic, amesema wembe ni uleule katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Maafande wa Mgambo JKT.
Kikosi cha Wekundu wa Msimbazi hao, Simba, tayari kimeshawasili jijini Tanga kwa ajili ya mchezo huo utakaochezwa kesho Uwanja wa Mkwakwani.
Akizungumzia mchezo huo, Goran alisema amefanya maandalizi mazuri katika kikosi chake, huku akiwapa majukumu wachezaji wake kuhakikisha wanarudi jijini Dar es Salaam wakiwa na pointi tatu mkononi.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhwzY40GVWdUMBiv-mcUskOFeylmb1rWIVhPHojNVI_8WyamtS5F8oGQY_lcrY2sdG57nCoWw5BdK2WokfhQcZ74A-VNfRusBjEPOWXfzIRYp3JtYxAGGfQ9ewtC4AyE0R-V9DBl8xZhco/s1600/1.jpg
Alisema ametumia siku mbili kwa ajili ya kufanyia kazi kasoro zilizojitokeza katika mchezo uliopita dhidi ya Mtibwa Sugar, hivyo tayari kikosi chake kipo imara kuwavaa Mgambo.
“Kila mtu anafahamu jukumu lake, tumepata ushindi katika mchezo dhidi ya Mtibwa, hivyo pia tunakwenda kwa wapinzani wetu tukiwa na akili ya kutaka kupata ushindi,” alisema.
Goran alisema anatambua anakutana na timu ngumu na kutumia vyema uwanja wa nyumbani, lakini kwa upande wake atahakikisha vijana wake wanatimiza majukumu aliyowapa.
“Kila mmoja anatambua jukumu lake, kwa hali hiyo tayari nimeshaandaa kikosi cha ushindi kwa kufikia malengo ya timu kumaliza katika nafasi za juu au kutwaa ubingwa,” alisema kocha huyo.-bingwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4