Watuhumiwa sita wa ugaidi wapandishwa kizimbani


WATU sita wanaotuhumiwa kujihusisha na vitendo vya ugaidi kwa kutegesha na kulipua mabomu yaliyotengenezwa kienyeji katika matukio matatu tofauti mkoani Ruvuma, jana wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma kujibu mashtaka yanayowakabili huku nje kukiwa na ulinzi mkali wa Jeshi la Polisi.http://anchortechnologies.com/wp-content/uploads/2013/05/Law-Photo.jpg



Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Simoni Kobelo,

Mwendesha Mashtaka ambaye pia ni

Wakili Mfawidhi wa Serikali wa Kanda ya

Ruvuma, Silivanus Mkude, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Juma Kibwana maarufu kwa jina la Msabila, Mwalimu Yusuph na Hamza Singano ambao ni wakazi wa Majengo, Manispaa ya Songea, Yasin Musa maarufu kwa jina la Kafupi ambaye ni mkazi wa Manispaa ya Songea, Hasan Mponda na Said Mhando.



Wakili Mkude alidai mahakamani hapo kuwa washtakiwa wote wanakabiliwa

na mashtaka matatu tofauti ya kujaribu kuwaua askari polisi waliokuwa doria na askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani waliokuwepo kazini katika eneo la Mshangano Manispaa ya Songea.



Alidai kuwa kosa la kwanza la kujaribu kuua lilitokea Desemba 25, mwaka jana katika eneo la Mtaa wa Kotazi Majengo na mmoja kati yao alijaribu kuwarushia askari polisi bomu lililotengenezwa kienyeji waliokuwa wanafanya doria na kabla hajafanikiwa lilimlipukia na kumsababishia kifo na askari polisi wawili walijeruhiwa.



Alitaja shtaka la pili kuwa Oktoba 27, mwaka jana saa 10 jioni walichimbia ardhini bomu la kienyeji katika eneo la Mshangano kando kando ya barabara ya kutoka Songea kwenda Njombe ambalo hutumiwa na askari wa Usalama Barabarani kama kituo cha ukaguzi wa magari yanayotoka na kuingia Songea Mjini kwa lengo la kuwalipua askari na kabla hawajatimiza lengo lao askari waligundua na kulitegua bomu hilo.



Alilitaja shtaka la tatu linalowakabili kuwa inadaiwa Septemba 16, mwaka jana saa 12 jioni katika Kata ya Misufini karibu na Matarawe Songea Mjini, waliwarushia bomu la kienyeji askari waliokuwa kazini na kuwajeruhi.



Kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi za ugaidi, washtakiwa hawakuweza kujibu mashtaka yanayowakabili na kesi hiyo itatajwa tena Februari 19, mwaka huu na washtakiwa wote wamepelekwa mahabusu baada ya kukosa dhamana.-Mtanzania

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4