Twiga Cement chafungwa muda usiojulikana

Kiwanda cha saruji cha Twiga Cement cha jijini Dar es Salaam, kimepigwa marufuku kuzalisha sementi kutokana na kusambaza vumbi la linalohatarisha afya za watu na kuchafua mazingira.
Amri ya kukifungia kiwanda hicho kwa muda usiojulikana  ilitolewa jana na Baraza la  Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) na kukiagiza kulipa faini ya Shilingi milioni 50 kwa kuvunja sheria.
 
‘Twiga Cement’ kwa mujibu wa NEMC inachafua mazingira na imeshindwa kudhibiti vumbi linalotokana na uzalishaji wa sementi linalopitia kwenye bomba lililoelekezwa angani.
Kiwanda hicho cha Twiga Cement ambacho kipo eneo la Wazo Hill nje kidogo ya Dar es Salaam kinahusishwa na kutodhibiti vumbi linalosaabisha watu kupata maradhi.
Kiwanda hicho kiliamriwa kulipa  mara moja faini ya Shilingi  milioni 50 kwa kuvunja kifungu namba 191 cha sheria ya mazingira ya mwaka 2004.
Kifungu hicho  kinasema yeyote ambaye atachafua mazingira kwa namna yoyote atachukuliwa hatua ikiwemo kufungiwa kiwanda pamoja na kulipa faini.
Akizungumza na wanahabari wakati akikifungia kiwanda hicho, Mwanasheria wa NEMC, Heche Suguta alisema  wamepokea malalamiko mengi kutoka kwa wakazi ambao wanakizunguka kiwanda hicho pamoja na wafanyabiashara wadogo wadogo wakilalamikia vumbi hilo kuathiri afya.
Alisema baraza lilijulishwa kuwa uchafuzi unaofanywa na kiwanda hicho umesababisha watoto kupata mafua yasiyoisha, kukohoa, kuumwa vichwa na Kifua Kikuu (TB).
Walilalamikia wakati mwingine kushindwa kulala.
Heche alisema vumbi hilo ambalo ni la saruji limesababisha matatizo mengi kwa wananchi na kwamba  hawapo tayari kuona watu wakiendelea kupata shida.
“Tumeamua kukifungia kiwanda hiki kikubwa cha Cement cha Tanzania ili iwe fundisho kwa viwanda vingine ambavyo vina tabia ya kukaidi maagizo ya serikali,” alisema Aliwaambia wanahabari kuwa  endapo kiwanda hicho kitakiuka agizo hilo polisi na NEMC watamkamata Mkurugenzi wake na utaratibu mwingine wa kisheria utaendelea.
Alieleza kuwa kabla ya kukifungia kiwanda hicho jana walituma wataalamu kwenda kuchunguza suala hilo ili kubaini hali ya  wanaathirika.
Wataalamu hao walithibitisha kuwa  kiwanda hicho kinatoa vumbi lenye athari kiafya na hatua ya kukifungia ilichukuliwa.
Awali Mkurugenzi wa Twiga Cement , Alfonso Rodriguez, alisema bomba ya kupitishia vumbi la saruji la kiwanda kipya limeharibika, hatua iliyowalazimisha  kutumia la kiwanda cha zamani ambalo limeelekezwa angani.
Alisema  kiwanda hicho kinafanya marekebisho ya kasoro hiyo.
 -NIPASHE

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4