Tanzania, Ufaransa waanzisha kundi la kirafiki

UBALOZI wa Ufaransa nchini umeanzisha kundi la kirafiki kati ya Tanzania na Ufaransa, kwa ajili ya kubadilishana uelewa katika masuala mbalimbali ikiwemo siasa, sayansi, utamaduni na uchumi.
Balozi wa Ufaransa nchini, Bertha Semu-Somi, alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake Mjini Dar es Salaam.
Alisema kikundi hicho kitazinduliwa rasmi Februari 20, mwaka huu nyumbani kwa balozi na kwa kuanzia kitakuwa na wajumbe 50 ambapo baadaye wataendelea kuongezeka.
“Wajumbe wa kikundi watakuwa wanakutana mara tatu kwa mwaka kwa ajili ya kubadilishana mawazo na ujuzi, ajenda mbalimbali zitajadiliwa zikiwemo za kisiasa, elimu na uchumi.
Alisema wapo Wafaransa wanaohitaji kuijua zaidi Tanzania na wapo Watanzania wanaohitaji kujua utamaduni wa Wafaransa, hivyo kupitia kikundi hicho kila upande utanufaika.
“Lengo ni kuunganisha watu tofauti tofauti, kundi litakuwa uwiano sawa kati ya wanawake na wanaume wa Kitanzania na Ufaransa kwa ajili ya maendeleo,”-MTANZANIA

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4