Simba yairuka kimanga Fifa

BAADA ya Simba kuagizwa kumlipa beki Donald Mosoti takribani dola za Kimarekani 14,400 kwa kusitisha mkataba, klabu hiyo imesema haijapokea barua yoyote inayowataka kufanya hivyo.http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/10/Flag_of_FIFA.svg/2000px-Flag_of_FIFA.svg.png

Simba ilimsainisha Mosoti mkataba wa miaka miwili na nusu akitokea Gor Mahia ya Kenya, ambapo alicheza nusu msimu na kutupiwa virago vyake, ndipo akaamua kupeleka madai yake Shrikisho la Soka Ulimwenguni, Fifa, kwa lengo la kudai haki zake.

Juzi Fifa ilitoa uamuzi wa kuitaka klabu ya Simba kulipa fedha hizo kwa muda wa siku 30 zijazo pamoja na riba ya asilimia tano ya malipo yake kwa mujibu wa uamuzi uliofikiwa na majaji.

Katibu Mkuu wa Simba, Stephen Ally, amesema bado hawajapokea barua kutoka Fifa inayoagiza kumlipa beki wao wa zamani, hivyo watakapopata watatolea uamuzi na kuliweka bayana.

“Kwa sasa ni mapema kuzungumzia suala hilo, bado hatujapewa barua kutoka Fifa, hivyo tunasubiri barua na baada kuona inavyoeleza tutajua nini cha kufanya,”

Simba walimtema Mosoti, ambaye alikuwa kipenzi cha mashabiki kutokana na kiwango alichokionyesha kwa muda mfupi tangu kusajiliwa kwake ili kupisha usajili wa Emmanuel Okwi, aliyekuwa akiichezea Yanga.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4