Mbeya City yapangua adhabu ya TFF kwa Nyosso

KOCHA Mkuu wa kikosi cha Mbeya City, Juma Mwambusi, ni kama amepinga adhabu aliyopewa beki wake, Juma Said ‘Nyosso’ na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), baada ya kusema ni kubwa na ni kama wameidhulumu timu.
Kauli hiyo imekuja ikiwa ni siku chache baada ya TFF kutoa adhabu ya kumfungia beki huyo kucheza mechi nane kwa kosa la kumshika makalio straika wa Simba, Elias Maguli.
Nyosso alidaiwa kutenda kosa hilo la udhalilishaji katika mchezo wao dhidi ya Wanamsimbazi, uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, ambapo wagonga nyundo hao wa Mbeya waliweza kuibuka na ushindi wa 2-1
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjte924qbwJFlqPUljvr3_izT0WnVf_bFGmPXd3vwnP-UmXeCPNt8xvwSOrODrNeuhB0SuIPtjXgDOlmHCGzPBXDKebkoOemZPa2uFi8fr25YFzJ8bVNbxKf6cG49PRFb9cJJsljnnanK4/s1600/Nyosso2.JPG
Mwambusi alisema adhabu aliyopewa mchezaji wake ni kubwa, kwani ni sawa na kutocheza mechi za mzunguko mzima, kitu kinachoweza kuigharimu timu.
“Ukweli sijui kanuni gani zimetumika katika hili, ni bora TFF waziweke wazi, kumsimamisha mchezaji michezo nane ni sawa na mzunguko mmoja, bora wangemtoza faini ya pesa, huko ni kuua kiwango cha mchezaji mwenyewe pamoja na kutoitendea haki timu, ukizingatia tulimsajili kwa kipindi kifupi,” alisema Mwambusi.
Wakati huo huo, uongozi wa wagonga nyundo hao umepanga kukata rufaa kupiga adhabu iliyotolewa.
Msemaji wa Mbeya City, Dismas Ten, alisema wapo katika mchakato wa kukata rufaa TFF, kwani maamuzi yaliyotolewa hayakuangalia pande zote, kwa maana ya mchezaji, timu anayoitumikia na aliyetendewa kosa.
“Kuanzia kesho tutawasilisha rufaa yetu TFF kupinga maamuzi yaliyotolewa na Kamati ya Maadili, siyo kwamba tunatetea vitendo vya utovu wa nidhamu, hatukumtuma Nyosso kutendea kosa lile, sasa kumsimamisha mechi nane ni sawa na kuihukumu timu isimtumie, ni heri angetozwa faini,-bingwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4