Watendaji waswekwa rumande

MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Magessa Mulongo, ameanza kazi kwa  kuwaweka  rumande baadhi ya madiwani na  watendaji wa halmashauri za wilaya  kutokana na kutofautina  kauli ndani ya vikao.
 Mulongo alikabidhiwa ofisi Novemba 25  mwaka huu akitokea Arusha.  Amekwisha kuwatangazia viongozi wa jiji la Mwanza kuwa hatafanya kazi na watumishi wazembe wanaoendekeza porojo za  siasa   badala ya vitendo.http://www.travelotanzania.com/images/destination/1365068692_1!!-!!Mwanza.JPG
 Katika kikao cha kwanza  kilichohusisha mameya, wakurugenzi wa halmashauri zote, wakuu wa idara, wakuu wa wilaya na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa, aliwaamuru mameya na wakurugenzi wa halmshauri kueleza sababu za Jiji la Mwanza kupata hati chafu    na akataka ripoti ya utekelezaji wa agizo la Rais Jakaya Kikwete la ujenzi wa maabara.
Baada ya  maelezo ya viongozi hao,  RC Mulongo amesema   anasikitishwa    kwa kitendo cha viongozi wa mkoa huo kumdanganya kwa kumpatia taarifa ya  maandishi ambayo haina uwiano na maelezo yao na kuwaita kuwa ni viongozi mfilisi walioagana na Serikali.
 “Nimegundua taarifa niliyokabidhiwa ya kila wilaya ni ya uongo kwa sababu ukweli nimeujua hapa kwa maelezo yenu; kwanza majibu yenu ni ya siasa, hayajitoshelezi, nimegundua viongozi wengi wanaligharimu taifa na wengine hawajui wajibu wa nafasi zao.

“Kwa maelezo yenu hapa, nimegundua hapa Mwanza kuna viongozi wazembe, nisema wazi wengi wenu mtaondoka na ujenzi wa  maabara na hati chafu yenu, haiwezekani nyaraka zikapotea wakati wa ukaguzi.
 “Hakuna mtu anayefanya kazi ya mwingine wakati mwenyewe yupo, sitaki visingizio katika utekelezaji wa majukumu anayeona haendani na kasi aondoke mapema, sitaki hati chafu tena, pia naomba wakurugenzi na watumishi wengine sitaki fujo,wengi wenu nimeambiwa mnayo miradi binafsi wananchi wanateseka wakati nyie mnacheka,”.
Mulongo ambaye alianza ziara ya kutembelea wilaya Novemba 2, ikiwa ni siku ya pili tangu kukabidhiwa ofisi hiyo  na kuanzi Wilaya ya Misungwi ambako aliingia  mgogoro na watendaji wawili ndani ya kikao baada ya kutofautiana kauli kuhusu ujenzi wa maabara kitendo kilichosababisha kuagiza kukamatwa na kuwekwa rumande.
 Pia Mulongo amehitilafiana na Diwani wa Chadema Kata ya Mbungani Wilaya ya Nyamagana, Hassan Kijuu, ambaye alimtaka mkuu huyo kutokuwa mbabe na kutowafanya kama watoto na badala yake anatakiwa kuheshimiana katika kazi.

Mulongo alizidi kukasirishwa na diwani huyo  baada ya kumweleza kuwa hakuzingatia muda wa kikao kilichoanza saa 3.00 asubuhi lakini yeye aliingia saa 6.00 mchana.
   RC   aliingia mgogoro mwingine  na watendaji na madiwani wilayani Ukerewe juzi na kuagiza askari kumkamata diwani wa Chadema na kumuweka rumande  baada ya kutofautiana kauli juu ya ujenzi wa maabara.
 Kutokana na migogoro hiyo, hivi sasa Rc Mulongo anatembea na askari wawili wa ulinzi na wakati mwingine  kuongozwa na  pikipiki za  ving’ora kwa kile kinachoelezwa ni kuhofia usalama wake.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4