Wanne mbaroni kwa mauaji

JESHI la Polisi mkoani Pwani linawashikilia watu wanne wanaodaiwa kujihusisha na uchochezi wa vurugu  na mapigano ya jamii ya wafugaji yalitokea Novemba 26 katika Kijiji cha Kihale Tarafa ya Chole wilayani Kisarawe   na kusababisha mauaji ya watu tisa.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani,   Ulrich Matei, ametoa ufafanuzi huo alipozungumza na waandishi wa habari  kuhusiana na tukio la mapigano ya wafugaji   Wasukuma na Wabarbeig.http://1.bp.blogspot.com/-nknbe6JQTyk/T2-ihTNOqEI/AAAAAAAAAj0/RZFkC-HsqAE/s400/Police1.jpg
 Matei  amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni  Chacha Mganja (24), Kidaini Kidatu (20), Musa Bohai (20)  na Emmanuel Kihuga (29)  ambao kwa pamoja wanadaiwa kuwa   chanzo cha mapigano hayo.

Amesema pamoja na kukamatwa kwa watuhumiwa hao lakini bado Jeshi hilo linaendelea na msako mkali wa kuhakikisha wengine waliohusika katika tukio hilo wanatiwa nguvuni lengo likiwa ni kutaka kuimarisha usalama wa maeneo husika na hata kudhibiti vitendo hivyo visitokee maeneo mengine.

Matei amesema   mpaka sasa watu sita waliouawa katika mapigano hayo wametambuliwa na tayari madaktari wamewafanyia uchunguzi na  kukabidhiwa kwa ndugu zao kwa mazishi.  Hao ni  Sarafu Samson (18), Njili Juma (20), Kajilo Naelomi (27), Daniel Nyerere (30), Pascal Matias na Alex Kiteu  (21).

“Mapigano hayo yalitokea Novemba 26 asubuhi katika Kijiji cha Kihale baada ya Alex Kiteu ambaye ni Mbarbeig kuiba ng’ombe 51 mali ya Doto Charles.  Katika  msako Kiteu alikutwa akiwa na ng’ombe hao na hivyo Wasukuma wakamuua kwa kutumia mapanga, mikuki na mishale,”

Amesema baada ya Wabarbeig kuona mwenzao ameuawa siku ya pili walilipiza kisasi kwa kutumia mishale, mikuki na mapanga kufanya mashambulio na kuwaua Wasukuma ambao inadaiwa walikuwa sita .

Kutokana na mapigano hayo Mkuu  wa Mkoa wa Pwani, Mwantum Mahiza, amewataka wafugaji walioingia mkoani  Pwani bila kufuata utaratibu waondoke haraka na kama watashindwa kufuata maagizo yake watakaokamatwa watachukuliwa hatua kali za  sheria.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4