Viongozi wa dini washauriwa kwenda shule

VIONGOZI wa dini nchini wametakiwa kwenda shule kusoma masomo ya kijamii badala ya kung’ang’ani ya kidini pekee hali ambayo husababisha waumini wengi wasiwe na ufahamu wa kuzijua sheria na haki zao za msingi ndiyo maana wamekuwa wakionewa na kupoteza haki zao.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Mchungaji Anna Suguye wa huduma ya The Word of Reconciliation Ministries (WRM) ya jijini Dar es Salaam wakati wa mahafali ya 26 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika Bungo Kibaha mkoani Pwani.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjabR3cbSh1SJIKiIDjGwEoIVGVxCJF6US-EtaqxcgS2y7Pp_jG-NZhG0x1uQB8Q2jrZfW3QewgXzEC4urzvHD1qJrgGeOTKsskFq8oliXYoDkc3YSROZKqNb5mxvU_AAkLz2n4dFguXaYV/s1600/p1.jpg
Anna ambaye amehitimu Shahada ya Usimamizi wa Biashara na Uongozi wa Rasimaliwatu alisema ni vizuri viongozi wa dini kusoma masomo ya kijamii ambayo pia yanaweza kuwasaidia waumini wao kwani watakuwa na uelewa mpana wa kuwaongoza waumini wao.
“Kuna viongozi wengi wa dini hawajui sheria za kuwaongoza watu wanaowahudumia na ndiyo maana wamekuwa wakitoa mafundisho ya kuwapotosha watu wao jambo ambalo ni hatari kwa taifa,”alisema Anna.
Aidha, Anna alisema kwa baadhi ya viongozi wa dini hufikiri kusoma masomo ja kijamii ni dhambi na badala yake wanang’ang’ana na elimu ya kidini pekee na kuongeza kwamba kiongozi mzuri ni yule aliyesoma elimu zote mbili kwa manufaa ya anaowaongoza.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4