Tohara yaharibu Sherehe za Ukimwi

MAADHIMISHO ya  Siku ya Ukimwi wilayani Tarime yalidorora baada ya wananchi kutofika eneo husika na badala yake  kwenda kwenye sherehe za jadi za tohara kwa wanaume  na watoto wa kike.
Tuklio hilo lilitokea   Kijiji cha Nyamwaga ambako maadhimisho ya Ukimwi yalifanyika.  
Kutokana na tukio hilo  aliyekuwa mgeni rasmi, Ofisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Tarime, Victir Kabuje, alisema alisikitishwa na kitendo cha wananchi kutothamini elimu ya Ukimwi na kukimbilia sherehe za ukeketaji.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhnGCEi8kGOvX5J4p59DMegLs_19_Njg9cvyNd5VzKn6WlTli_S3QM_y0VnGtiAHwgBHdvi82_9Wd-TsEIySevS_rE1oSFL_37FMEznk8epKIu-eIUhSSEPrBvJrMP6gmHaNv-BieiJ6tg/s1600/01.tarime12.jpg
Kabuje ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya  Tarime, John Henjewele, aliwaasa wananchi hao kuacha kukeketa wasichana bali tohara ifanyike kwa wanaume pekee
Hata hivyo Kabuje alimtupia lawama Mwenyekiti wa  Kijiji cha Nyamwaga, Kirigiti Sasi kwa  kushindwa kuhamasisha wananchi kujitokeza kwenye maadhimisho ya Siku ya Ukimwi.
Aliwaasa  wananchi kuacha mila potofu ili kuendana na wakati.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4