Simba yawaanika wauaji wa Express


MSHAMBULIAJI mpya wa timu ya Simba, Mganda Dan Sserunkuma leo anatarajia kuongoza mashambulizi ya timu hiyo itakapovaana na Express ya Uganda.
 Sserunkuma alitua nchini juzi na tayari amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia timu hiyo, akitokea Gor Mahia ya Kenya aliyomaliza nayo mkataba.
 http://www.soka25east.com/wp-content/uploads/2014/12/Gor-Dan-Sserunkuma-high-300.jpg

Mganda huyo ambaye ni mfungaji bora wa Ligi Kuu Kenya msimu uliopita kwa mabao 16, ni tegemeo jipya la ushambuliaji kwenye kikosi hicho akisaidiana na Mganda mwenzake Emmanuel Okwi.
Mchezo huo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam unatarajia kuanza majira ya saa 11 jioni.

Kocha mkuu wa Simba, Patrick Phiri atautumia mchezo huo kwa ajili ya maandalizi ya mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Yanga Desemba 13, mwaka huu.

Express inayoshika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini Uganda, tayari imeshatua nchini kwa ajili ya mchezo huo na ule wa Yanga itakayopambana nayo kesho.

Wachezaji wapya wa Simba ambao nao huenda wakawemo kwenye mchezo huo ni mshambuliaji Danny Mrwanda, aliyetokea Polisi Morogoro, huku kiungo Omar Mboob naye akitarajia kujaribiwa.

Mboob raia wa Gambia yupo kwenye majaribio ndani ya kikosi hicho tokea mwanzoni mwa wiki hii, hiyo ni baada ya Phiri kupendekeza atafutwe kiungo wa kuongeza nguvu katika kikosi hicho.Displaying simba.JPG

Simba iliyoanza vibaya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa kuambulia ushindi wa mchezo mmoja na sare sita, ipo kwenye mawindo ya kuimarisha kikosi chake ambapo kwa sasa inafukuzia kipa, kiungo na beki wa kati.

Kipa anayedaiwa kuwa mbioni kujiunga na wekundu hao ni kipa wa zamani wa timu hiyo, Juma Kaseja aliyegoma kurejea kwenye timu yake ya Yanga baada ya kutofautiana na uongozi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4