RC awa mbogo kwa wakurugenzi Mwanza

MKUU wa Mkoa  wa Mwanza, Magessa Mulongo, juzi  aliugeuza ukumbi wa mikutano kuwa mahakama baada ya kuwaweka kiti moto wakurugenzi, mameya, wenyeviti wa wilaya na watumisshi wengine kueleza sababu ya Jiji la Mwanza kupata hati chafu ya hesabu na kukithiri kwa migogoro.
Pia aliwataka kueleza hatua ya utekelezaji wa agizo la Rais Jakaya Kikwete la ujenzi wa maabara tatu katika kila shule ya sekondari ifikapo Novemba 30 kitendo ambacho kilifanya baadhi ya watendaji kushindwa kuzungumza.
Mulongo juzi alipokewa na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Baraka Kinisaga na niaba ya aliyekuwa mkuu wa mkoa  huo, Evarist Ndikilo aliyehamishiwa Arusha na kukabidhiwa ofisi  hiyo rasmi
http://media2solution.files.wordpress.com/2012/05/magesa-mulongo.jpg
Magessa Mulongo
Aligeuka  mbogo kwa watendaji wa mkoa huo ikiwa ni muda mchache baada ya kukabidhiwa taarifa ya kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo.
Alianza kuwasimamisha wenyeviti wa wa kila wilaya na wakurugenzi wa halmashauri ambazo ni Ilemela, Nyamagana, Ukerewe, Misungwi, Magu, Sengerema  na Kwimba, kueleza sababu za kuwapo hati chafu Jiji la Mwanza ambako maelezo yao kwa asilimia 90 yalifanana wakisingizia kupotea kwa nyaraka.
Sababu  nyingine ni zilizotolewa na watendaji hao ni kwamba Jiji la Mwanza lilipata hati chafu kutokana na kukosekana ushirikiano kati ya wahasibu na wakaguzi  kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), kutokamilika miradi mingi ya maendeleo na wakurugenzi kujichukulia uamuzi bila kushirikisha wahusika.
Kwa upande wa maabara, hakuna wilaya hata moja ambayo itatimiza agizo la Rais la kuwa na maabara ifikapo Novemba 30 mwaka huu kwa sababu majengo yapo kwenye boma huku shule nyingine zikiwa hazijaanza ujenzi.
Sababu zilizoelezwa kukwamisha shughuli hiyo ni baadhi ya viongozi wa siasa kuhamasisha wananchi kutochangia, migogoro ya ardhi, ukosefu wa fedha na mambo mengine mengi.

Kutokana na maelezo hayo, Mulongo alisema  anasikitishwa   kwa kitendo cha viongozi wa mkoa huo kumdanganya kwa kumpatia taarifa ya  maandishi ambayo haina uwiano na maelezo yao na kuwaita kuwa ni viongozi mfilisi walioagana na Serikali.
Mulongo alisema hataki kufanya kazi na wakurugenzi wanaolalamikiwa na wananchi huku akuiwataka kuwatumia mgambo kama chambo kwa wanachi, pia alikataa wananchi kunyang’anywa bidhaa zao huku akitoa tahadhari kwa jeshi la polisi kutumiwa vibaya na viongozi kuhatarisha amani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4