Ray C: Ofa zilinivurugia ndoto zangu

MREMBO  mwenye kujishughulisha na muziki wa Bongo fleva nchini, Rehema ‘Chalamila ‘Ray C’, amedai kuwa ndoto zake za  kuwa Dj mkubwa hapa nchini, zilivurugika  baada ya kupata ofa ya kuimba na kurikodiwa wimbo mmoja bure.
 Awali kimwana huyo, aliwahi kuwa mtangazaji wa kituo kimoja cha radio hapa nchini, alisema baada ya kurikodi wimbo huo, mapokezi yake yalikuwa mazuri na hatimaye kuongezewa ofa ya albamu nzima bure hali iliyomfanya asitishe kabisa utangazaji na kujitumbukiza katika ulimwengu wa sanaa ya muziki wa bongo fleva.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgAg0h0hcU2cUvuXUddt-i5IfiYeqPHhJeD9TxCWw1_PrAY02Iok9rDz2PQIKfqmDs4crj6BM9Ir-Z4V04gWVYASxH5zQJ31KOGUCWyMrTkdXL6sBVzCYYXahoGHUjYqC5zTwnGBeFsm6rO/s1600/rAY+c+sICKNESS.jpg
“Nakumbuka nilikuwa mtangazaji na DJ mzuri tu hapa nchini, lakini kutokana na kuwa na kipaji kingine cha kuimba na watu walikitambua, ilinibidi nisitishe kitu kimoja na kuegemea zaidi kwenye muziki kwasababu tayari mapokezi ya mashabiki yalikuwa ni ya kutisha,”Ray C.
Anasema anawaomba mashabiki wake waendelee kumpa sapoti katika kile anachookifanya, pia yuko njiani kuachia ngoma mpya zitakazo rudisha heshima na hadhi yake ya kipindi cha nyuma alichokuwa akishindanishwa na mkali wa bongo fleva Lady Jdee.
“Nakumbuka enzi zangu nilikuwa nashindanishwa na wasanii wakubwa lakini sasa ushindani umekuwa tofauti kabisa, nawaahidi mashabiki wangu wote kuwa letea burudai wanazozihitaji ambazo zitarudisha ata heshima yangu katika hii sanaa,”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4