Profesa Jay: Muziki wa sasa ni ajira si fani

MKONGWE wa  Hip Hop nchini, Joseph Haule ‘Profesa J’ amekiri juu ya muziki wa sasa kuwa ni ajira na si fani kama ilivyokuwa enzi zao miaka ya nyuma.
Mkongwe huyo aliyetamba na wimbo wake wa ‘Nikusaidieje’ anasema muziki wa sasa unaonekana kuwa ajira kutokana na vijana wengi kujitumbukiza katika tasni hii kwa ushindani wa hali ya juu huku kila mmoja akijaribu kumvuta mwenzake ili yeye awe juu.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiVN84xoDsp2103g48HmojqN258DruhBshjPhxDL6tC6gpQsUVShaCU3IJwh-J9LQ3cfwN228oIcDVZUUJqtGphzfhr7ki1V9bQBi1jQlggaBBk9K4AF6vZXmB866xO7ArDabBmiKyTghSK/s1600/PROF+jay.jpg
“Uanjua kunautofauti mkubwa sana kati ya muziki wa sasa na waenzi zetu, ukizingatia kila kukicha vijana wanaibuka katika muziki kama njia ya kujipatia ajira, tofauti na miaka ya nyuma ambayo tulikuwa tunaimbia fani,”
Anasema, hilo limeufanya muziki wa sasa kuonekana ni mwepesi wakati huo huo unaonekana kuwa mgumu kutokana na chipukizi wenye vipaji na mitindo tofauti tofauti wanayoibuka nayo kila kukicha kama ilivyo kwa Naseeb Abdul ‘Diamond Platnums’.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4