Phiri amrudisha Kaseja Msimbazi

KOCHA Mkuu wa Simba Mzambia, Patrick Phiri, amesema yupo tayari kufanya kazi na Juma Kaseja katika kikosi chake kwa kuwa anamjua vizuri na kwamba ni mmoja wa magolikipa wazuri hapa nchini.

Phiri amelazimika kuyaweka wazi hayo baada ya kuwa na taarifa za Wekundu hao wa Msimbazi kumrejesha kipa huyo ambaye kwa sasa anaichezea Yanga ili kuboresha kikosi chake.
http://www.ippmedia.com/media/picture/large/Kaseja2(11).jpg
Kaseja
Phiri anadai kulingana na upungufu uliopo katika nafasi ya kipa kwenye kikosi chake, hana budi kutaka kuongezewa kipa mwingine mzoefu ili kusaidiana na waliokuwepo katika kikosi hicho.
Simba inaendelea na mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, lakini inakabiliwa na upungufu mkubwa kwenye kikosi chake kutokana na kuwa na kipa mmoja tu kikosini, Manyika Peter, baada ya wengine wawili; Ivo Mapunda na Hussein Shariff kutokuwepo kutokana na kukabiliwa na matatizo tofauti tofauti.
Ivo hayupo kwa sababu anamalizia msiba wa mama yake mzazi wakati Sharrif yeye ni majeruhi.
Kutokana na hali hiyo, Phiri amesema anahitaji kipa mwingine wa nyongeza hivyo kama uongozi utaamua kumsajili Kaseja itakuwa furaha kwake ikizingatiwa kuwa golikipa huyo anaujua utamaduni wa Simba kutokana na kuichezea kwa muda mrefu.
"Kaseja ni mmoja wa wachezaji walioitumikia Simba kwa muda mrefu tena kwa mafanikio, hivyo nathubutu kusema anaujua utamaduni wa klabu hii, kama atakuja hatutapata tabu kwake kwani anajua kila kitu hapa," Phiri.
Phiranasema amepeleka mapendekezo ya kuongezewa kipa mwingine ili kusaidiana na waliopo ambapo japo hakuweka wazi kwamba anamtaka Kaseja lakini amesisitiza kuwa iwapo atakuja atafanya naye kazi, jambo ambalo linatafsiriwa kuwa bado anamuhitaji kikosini.
Unafuu kwa Simba unaweza kupatikana kutokana na kauli ya uongozi wa Yanga ambao ulikaririwa hivi karibuni kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya klabu hiyo, Seif Ahmed 'Magari' akisema kuwa klabu hiyo haina nia ya kumzuia kipa huyo endapo anataka kujiunga na Simba, lakini akasisitiza kuwa ni lazima taratibu zifuatwe.
Kaseja anataka kuondoka Yanga aliyojiunga nayo kwenye usajili wa dirisha dogo la msimu uliopita kutokana na kukosa nafasi ya kucheza, kwa vile kocha wa timu hiyo, Marcio Maximo amekuwa akimtumia Deogratius Munishi 'Dida' kama kipa wake namba moja.
Unaweza kutoa maoni yako hapo chini..

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4