Huruma yamponza ofisa

MAMLAKA ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Jijini Mwanza (MWAUWASA) imemsimamisha kazi Ofisa Raslimali Watu, Zacharia Membo,  kupisha uchunguzi wa tuhuma za kuajiri na kuwalinda watumishi   wasio na sifa za kupata ajira.

Uamuzi huo umefikiwa na kikao cha Bodi ya MWAUWASA kilichoongozwa na Mwenyekiti wake, Christopher Gachuma baada ya kupokea malalamiko katika kikao cha watumishi  wa mamlaka hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA,   Anthony Sanga, amethibitisha kusimamishwa kwa ofisa huyo
.http://www.mwauwasa.org/sites/default/files/styles/large/public/page/images/zandfilters_capripoint.jpg?itok=ITuz8XtB


Amesema hatua hiyo imechukuliwa kuupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili  baada ya kulalamikiwa na watumishi wenzake.


Taarifa za ndani toka MWAUWASA zimeeleza kuwa katika kikao hicho   watumishi   walilalamikia kitendo cha ofisa huyo kuwalinda watumishi wenye vyeti bandia licha ya kuarifiwa.

Inaidaiwa ofisa huyo licha ya kutambua watumishi hao kutokuwa na sifa bado amekuwa akiwachangisha fedha baadhi yao  kuwasaidia kulinda ajira zao.

Kutokana na malalamiko hayo Gachuma alimtaka Mkurugenzi wa MWAUWASA kumchukulia hatua kali za maadili ofisa huyo.

Amesema  watumishi wote watakaobainika kughushi vyeti nao wachukuliwe hatua ikiwamo kupendekeza kwa Waziri wa Maji watimuliwe kazi mara moja.

  Mkurugenzi Mtendaji wa MWAUWASA,   Anthony Sanga,  amesema ofisa huyo anatuhumiwa kutumia ofisi na wadhifa wake vibaya ikiwa ni pamoja na kujipatia fedha.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4