Mwanamke amuua mumewe katika ugomvi wa familia


MWANAMUME  mkazi wa mtaa wa Mkoani Kata ya Kalangalala wilayani Geita,  Kipara Ngw’endesha (46), ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito sehemu mbalimbali za mwili na mkewe kutokana na ugomvi wa  familia.
 Akizungumzia tukio hilo, mtoto wa marehemu, Regina Kipara (19), alisema  tukio hilo  lilitokea juzi   usiku baada ya mke wa mwanamume huyo,  Mwadawa Mussa, kumshambulia    kwa kutumia    mpati ambao hutumika kushikia sufuria wakati wa kupika chakula.http://www.mining-technology.com/projects/geita-gold/images/3-geita-mine.jpg

Regina alidai   chanzo cha mauaji hayo ni ugomvi wa familia uliosababishwa na hali ngumu ya  maisha inayoikabili familia yao.
 “Yaani huyu mama alikuwa akitaka kila anapotaka fedha apewe na ikitokea baba akasema hana anaanzisha vurugu,’’alisema.
 Regna alisema ilifikia kipindi baba yao aligoma hata kumtolea mahali kwa sababu  alikuwa ni kero katika  familia hiyo.
Alisema  kabla ya mauti kumkuta baba yao alikuwa na mpango wa kuachana mama yao  kutokana na vurugu zisizokwisha  alizokuwa akizianzisha mama yao huyo wa kambo.

 ‘’Unajua hali ya uchumi hapa nyumbani imeporomoka  kutokana na mikopo ambayo baba alikuwa amechukua kwenye taasisi za fedha  ndiyo maana hata mimi nimerudishwa shule sababu ya ada na baba aliniambia nimsubiri ajipange ndiyo niendelee na masomo yangu,”alisema.

 Mwenyekiti wa mtaa wa Mkoani ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kalangalala mjini Geita, Peter Donald, amethibitisha kuwapo   mauaji hayo na kwamba  tayari mwanamke huyo anashikiliwa na  polisi kwa hatua zaidi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Joseph alisema upelelezi wa tukio hilo unaendelea.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4