Muhuri wawaponza wagombea Chadema
Wagombea
hao 1,400 kutoka vijiji 56 vya jimbo hilo, walikutwa na dhahama hiyo baada ya
kuwekewa pingamizi na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya muhuri
waliotumia katika fomu za uteuzi wa wagombea kusomeka ‘CDM’ badala ya Chadema
kama ilivyozoeleka.

MUHURI
mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umewaponza wagombea wake
wote wa Serikali za Mitaa wa Jimbo la Meatu, mkoani Shinyanga.
Pamoja
na chama hicho kukata rufaa, Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa ambaye ni Katibu
Tawala wa Wilaya ya Meatu, alitupilia mbali rufaa hiyo hali iliyozua vurugu
kutoka kwa wanachama wa Chadema waliotaka mwenyekiti huyo kuwasomea rufaa hiyo,
badala ya kuwapa barua wakasome wenyewe kama alivyofanya.
Hatua
hiyo ilisababisha polisi kuwakamata Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa Shinyanga, Mwenyekiti
wa Baraza la Wazee, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Wilaya (Bavicha) na
viongozi wengine nane.
Mbunge
wa Meatu, Meshack Opurukwa (Chadema), alisema kilichofanywa na kamati ya rufaa
ni uonevu, kwani walioweka pingamizi si wagombea kama sheria zinavyosema.
“Pingamizi
lile ni batili kwa sababu waliokata rufaa ni wanachama, si wagombea na
wanaposema muhuri ule si wetu wanamaanisha nini? Wa kulalamika kuhusu uhalali
wa muhuri ni sisi, si Serikali wala mtu mwingine yeyote.
“Hatua
hii imesababisha wagombea wa CCM wanaowalinda kupita bila kupingwa na sisi
hatutakuwa na Serikali katika ngazi ya mtaa jambo ambalo si haki kwa sababu
walijua tutashinda kwa kishindo,” alisema Opurukwa.
Akizungumzia
sakata hilo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa, alisema chama chao kimewekewa
mapingamizi mengi, lakini batili jambo linalompa hofu kwamba kamati za rufaa
zinatekeleza maagizo waliyopewa kukiondoa chama hicho katika Serikali za mitaa.
Alisema
hatua ya kukataa rufaa za mapingamizi yanayowekwa ni kufanya mlolongo uwe mrefu
ili wakasirike na kwenda mahakamani ambako itachukua muda mrefu kutolewa uamuzi
jambo ambalo Chadema wanalipinga.
“Si
Meatu tu, tumewekewa pingamizi 500 Karagwe, hizi sababu zake ni wadhamini,
Mwanza 400 na Dar es Salaam 50, hii kwa Chadema haikubaliki sababu ya muhuri ni
hoja isiyo na mashiko,”.-Mtanzania
Maoni
Chapisha Maoni