Mshindi wa kwenda hifadhi ya Serengeri apatikana

KAMPUNI ya Bia ya Serengeti(SBL) imempata mshindi wa kwenda hifadhi ya Taifa ya Serengeti ikiwa ni droo ya pili tangu apatikane mshindi wa Bajaji limo kupitia shindano la kinywaji chake cha Serengeti Premium larger la ‘Tuitoke na Serengeti’ likiwa na lengo ni kuutangaza utalii wa ndani. Displaying 1.JPGMeneja wa Bia ya Serengeti, Rugambo Rodney (katikati) akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani wakati wa kuchezesha bahati nasibu ya shindano la Tutoke na Serengeti, linaloendeshwa na kampuni hiyo, ambapo Bw. Hassan Mfaume ameibuka mshindi katika Shindano hilo, kulia ni Msimamizi toka bodi ya michezo ya kubahatisha, Abdallah Hemedy na kushoto ni Auditor kutoka Pricewater House Coopers Ltd, Golder Kamuzora hafla hiyo imefanyika makao makuu ya Serengeti jijini Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam leo  Meneja wa SBL Rugambo Rodney amesema kuwa mshindi huyo ni Hassan Mfaume mkazi wa Mabibo na amepata  ziara ya kwenda kutembelea hifadhi ya taifa ya Serengeti.

amesema Hassan ambaye alikua kikazi Mwanza alionekana kushangazwa na kushitushwa baada ya kusikia taarifa kwamba amekuwa mshindi.

“Droo hii  imekuja wiki moja tu baada ya Rukia Almasi, ambaye ni Mama wa nyumbani na mkazi wa Kihonda-Morogoro kuibuka na  ushindi wa Limo Bajaj katika kampeni hii inayoendelea yenye lengo la kuutangaza utalii wa ndani,”

 Ameendelea kusema kuwa Hassan ameshinda safari ya watu wawili iliyolipiwa gharama zote na anaruhusiwa kwenda na mwenza wake, SBL watagharamia kila kitu kuanzia malazi, usafiri pamoja na vivutio mbalimbali.

Hata hivyo Rodney aliwasihi watanzania kuendelee kushiriki kwani zawadi za kushindaniwa zipo nyingi, kampuni imelenga katika kuinua utalii wa ndani ikiwa ni njia mojawapo ya kurudisha sehemu ya faida kwa wateja wake.Displaying DSC_3381.JPG

Amesema kampeni ya ‘Tutoke na Serengeti’ wameungana na B-Pesa wataalam wa teknolojia mpya ambao hivi karibuni wamezindua mfumo mpya wa usafirihaji wa fedha na  watahusika katika kusambaza fedha kwa washindi mbalimbali kote nchini kupitia simu za mkononi.



Pia amesema kuwa ili kushinda, unachotakiwa kufanya ni kununua bia ya Serengeti Premium Lager na angalia chini ya kizibo utakuta namba ambazo zinatakiwa kutumwa kwa ujumbe mfupi wa maneno (sms) kwenda namba 15317 ili kuingia katika droo.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4