Miaka 60 jela kwa kutorosha twiga

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Moshi mkoani Kilimanjaro leo imemhukumu miaka 60 jela, mshitakiwa wa kwanza raia wa Pakistani, Kamran Ahmed na kuwaachia huru Watanzania watatu katika kesi ya utoroshaji wanyama hai 153 wakiwemo twiga wanne.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi, Simon Kobelo, amesema baada ya upande wa jamhuri kufanikiwa kujenga kesi dhidi ya Mpakistani huyo kwa kiwango kisicho na shaka, mahakama hiyo imeridhika kwamba alitenda makosa yote manne yaliyowasilishwa dhidi yake.http://thetravelingmunschkin.com/wp-content/uploads/2012/10/Baby-Tembo.jpg
Kobelo amedai mahakama hiyo pia inaawachia huru Watanzania watatu, Hawa Mang’unyuka, Mathew Kimathi na Michael Mrutu kwa sababu upande wa jamhuri imeshindwa kujenga kesi dhidi yao na hata ushahidi uliowasilishwa hauoneshi kuwaunganisha washitakiwa hao moja kwa moja na kosa la kusafirisha wanyama hai nje ya nchi.
  
Katika hukumu hiyo, Kamran, alikutwa na makosa manne, kushiriki na kula njama ya kutenda uhalifu kinyume cha kifungu 57 (1), sehemu ya 4(1), sura ya kwanza ya kosa la uhujumu uchumi na kushiriki utoroshaji wa wanyama hai wenye thamani ya Sh 170, 575,500.

 Kosa la pili ni kufanya biashara ya kukamata na kusafirisha wanyama hai wakiwemo twiga, chui, ndege wa aina mbalimbali, duma, nyati, pofu, pundamilia na swala bila leseni.
Kosa la tatu ni kukutwa na nyara za Serikali katika Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), tukio lililotokea Novemba 26, 2010 na kosa la nne ni kuisababishia Serikali hasara ya Dola 113.7 za Marekani kwa kufanya biashara kinyume cha sheria.

Kuhusu kumuachia huru mshitkakiwa namba mbili, Hawa ambaye ni mmiliki wa Kampuni ya Harm Marketing na Luwego Bird Trappers inayodaiwa leseni yake kutumika kuhalalisha ukamataji na utoroshaji huo.
Hakimu Kobelo alidai kwa mujibu wa vielelezo vilivyowasilishwa ni wazi kwamba Harm ilipewa kibali halali cha kukamata wanyama hai na mamlaka husika hivyo mahakama hiyo inashindwa kumtuhumu moja kwa moja na utoroshaji huo.

“Ukirudi kwa mshitakiwa wa pili, jibu liko wazi, Hawa kupitia kampuni yake ya Harm Marketing alikuwa na leseni za kufanya biashara ya kukamata wanyama, baadaye kupitia mamlaka hizo hizo ziliruhusu mshitakiwa wa kwanza kufanya biashara hiyo hiyo kupitia Harm Marketing na katika kipindi hicho, Kamran aliendelea kutumia leseni hiyo mara kwa mara,” Kobelo.

Kwa upande wao, washitakiwa wa tatu na nne, Mathew na Michael kwa sababu hakuna sehemu yoyote inayoonesha ushiriki wao katika utoroshaji zaidi kutekeleza wajibu wao kama walivyoekezwa na wakuu wao wa kazi kipindi hicho.

Novemba 26, 2010, Kamran anadaiwa kuwatorosha wanyamka hai 153 wakiwemo twiga wanne kwenda Doha nchini Qatar kupitia KIA kutumia ndege ya jeshi namba C17, kinyume cha kifungu namba 84(1) cha Sheria namba tano ya Uhifadhi wa Wanyamapori ya mwaka 2009.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4