Mgombea CCM mbaroni kwa rushwa

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), inamshikilia kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwangwa Ephraim, kwa madai ya kupokea rushwa na kushindwa kurudisha fomu.
Kada huyo, alichukua fomu kwa ajili ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Kitongoji cha Kitagula, Kijiji cha Bumangi wilayani Butiama, lakini alishindwa kurudisha fomu yake Novemba 23, mwaka huu saa 10:30 kama ilivyopangwa.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEimCJuea7ZLKb_1cGQdcc9rQYXXLkEcnRvY5wTkauvUH-fNZye1wu6eCa4r8hu7DTj9LEiy-w9Qm7QCLDx-CE33QwKEgJMiRNVtGOiWjQGAM3Eqg7SnN9wEOv2GYALPb6fBr1pTKes_-m7n/s640/IMG_0295.JPG
Akizungumzia sakata hilo, Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mara, Holle Makungu, alisema kada huyo anadaiwa kupokea rushwa ya Sh 100,000 kutoka kwa mgombea mwenzake (jina linahifadhiwa) ili asirudishe fomu kwa muda uliopangwa ili mpinzani wake huyo apite bila kupingwa.
Makungu amesema uchunguzi uliofanywa na Takukuru unaonyesha kuwapo mazingira ya rushwa.
Mgombea huyo aliyepitishwa na chama chake, wakati wa kurudisha fomu ulipofika alizima simu ili kupoteza mawasiliano kwa viongozi wake hadi muda wa kurudisha fomu ulipomalizika.
“Tumefanya uchunguzi na kubaini mtuhumiwa alipokea rushwa kiasi cha Sh 100,000 kutoka kwa wakala wa mshindani wake toka chama shindani kwenye eneo hilo ili mgombea wake apite bila kupingwa.
“Kitendo hiki ni kinyume cha sheria na kinadumaza demokrasia ya vyama vingi, kwa kutumia rushwa kunawaondoa wagombea ambao wamepewa dhamana na vyama vyao,”  Makungu.
Hata hivyo, alisema uchunguzi zaidi wa tuhuma hizo bado unaendelea na mara utakapokamilika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtuhumiwa.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4