Meno ya tembo yamburuza kortini

MKAZI wa kijiji cha Lamadi wilayani  Busega, Madeni Nindwa (62), amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Magu akikabiliwa na mashitaka ya kukutwa na meno ya tembo yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 17.3 kinyume cha sheria.
Wakili wa Serikali Mfawidhi wa Mkoa wa Simiyu, Yamiko Mlekano pamoja na Mwanasheria wa Tanapa, Emmanuel Zumba, wamedai mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Magu, Robert Masige, kuwa mshitakiwa alitenda  kosa hilo   Novemba 26 mwaka huu. http://library.dbs.ie/Images/Site_Images/SubjectPortals/Law%20Portal.jpg
Mtuhumiwa   anakabiliwa na mashitaka  mawili ya kumiliki nyara za serikali ambazo ni meno ya tembo yenye thamani ya Sh 17,325,000   na kufanya biashara hiyo kinyume cha sheria.
Zumba amedai  mtuhumiwa   alikamatwa Novemba 26 mwaka huu   nyumbani kwa rafiki yake katika mji mdogo wa Lamadi wilayani Busega.
Alidai  mtuhumiwa huyo alikamatwa akiwa na vipande sita vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 18 vikiwa vimehifadhiwa kwenye mfuko  pamoja na mzani mmoja wa kupimia meno hayo.
  Zumba alisema    mashahidi  watakuwa   tisa na   upelelezi  umekwisha kukamilika.
Mtuhumiwa huyo aliyakana mashtaka yake na kupelekwa rumande  hadi Desemba 8 mwaka huu kesi yake itakapotajwa tena.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4