Mbaroni kwa kumnyonga mtoto

JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro, linamshikilia Zamir Shaban (27), mkazi wa eneo la Mkindo, Wilaya ya Mvomero kwa tuhuma za kumnyonga hadi kufa mtoto wake  wa kambo mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu.


Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Leonald Paul, alisema mauaji hayo yalifanyika Desemba 2 mwaka huu.



Alisema kwamba, mtuhumiwa huyo ambaye alikuwa mume wa mama wa mtoto huyo, Rehema Mustafa, inasemekana alimnyonga mtoto huyo kutokana na ugomvi wa kifamilia waliokuwa nao.



“Inasemekana kulikuwa na ugomvi kati yao uliopelekea mwanamke huyo kutafuta mume mwingine.



“Wakati wa mauaji hayo, mama wa mtoto huyo alikuwa amekwenda dukani kununua vitu na alimwacha mtoto wake huyo chumbani akiwa amelala.



“Mwanamke huyo aliporudi alimkuta mtoto wake akiwa amelegea na alipotoa taarifa polisi, mtuhumiwa alikamatwa na alipohojiwa alikiri kumnyonga mtoto huyo kutokana na mgogoro uliokuwapo kati yake na mkewe,” alisema Kamanda Paul.



Kutokana na hali hiyo, alisema mtuhumiwa ataendelea kuwa rumande hadi atakapofikishwa mahakamani baada ya taratibu za kisheria kukamilika.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4