Maximo aongeza dozi Yanga

KOCHA Mkuu wa Yanga Mbrazil, Marcio Maximo,ameamua kutoa ‘full’ dozi ya mazoezi ya kikosi chake kwa kuwaita pembeni kwa mafungu wachezaji wake na kuwaambia waache masihara kwani ndio wanaotegemewa kuibeba timu hiyo.
Yanga inaendelea na mazoezi katika Shule ya Sekondari Loyola jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kujiandaa na mechi zijazo za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara pamoja na zile za Nani Mtani Jembe.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZ8tueVThxTBUiolVx-Nn_NxXp8K3cN4leOXfrwNuirFazkXyMVuICbf563P3xqtXi8IhHGmjjSeYzU4a1FPqupDjsA_vGJ8HWD2rLfNgzWz6KM1gih2Ysst_bIgD5DbbNDj4I4HdLP0s/s1600/IMG_9242.JPG
Jana Maximo alianza kuwaita 'chemba' mastraika wa timu hiyo; Jerryson Tegete, Said Bahanuzi pamoja na Hamis Kiiza na kuwapa darasa kabla ya kuhamia katika idara nyingine.
Mbali na hilo, kocha huyo pia aliamua kupanga kabisa wachezaji wa kupiga penalti na wale watakaokuwa na jukumu la kupiga mipira ya faulo katika mazoezi ambayo yalifanyika Uwanja wa Shule ya Sekondari Loyola jijini Dar es Salaam.
Maximo anajua kwamba anakabiliwa na mchezo mgumu wa Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba Desemba 13 mwaka huu Uwanja wa Taifa ambapo hataki kufanya makosa yaliyofanywa na Ernie Brandts, aliyekuwa kocha wa Wanajangwani hao walipokubali kichapo cha mabao 3-1 msimu uliopita katika mchezo kama huo.
Katika mazoezi hayo Maximo alianza kuwapa wachezaji wake mazoezi ya kupasha moto misuli na baadaye kuwafundisha namna ya kuunganisha krosi, zoezi lililofanywa na wachezaji kwa ustadi mkubwa.
Baada ya Mbrazil huyo kuridhika na zoezi hilo aliamua kugawa vikosi viwili ambapo cha kwanza kiliongozwa na Deogratius Munish 'Dida,' Juma Abdul, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Nadir Haroub 'Cannavaro,' Haruna Niyonzima, Simoin Msuva, Andrey Coutinho, pamoja na Jerryson Tegete.
Kikosi cha pili langoni alisimama Aly Mustafa 'Barthez,' Salim Telela, Omega Seme, Rajab Zahir, Emerson De Oliveira, Mrisho Ngassa, Hasan Dilunga, Nizar Khalfani, Said Bahanuzi, pamoja na Mganda Hamis Kiiza.
Wachezaji hao walionyesha kandanda la kuvutia kutokana na maelekezo ya kocha wao ambapo hadi yanamalizika timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1, bao la kikosi cha kwanza lilifungwa na Msuva na la kikosi cha pili likifungwa na Said Bahanuzi.
Baada ya kumalizika zoezi la kucheza mpira ndipo likaja zoezi la upigaji penalti ambapo waliopewa jukumu hilo walikuwa ni Cannavaro, Joshua, Msuva, Tegete, Bahanuzi, Ngassa, pamoja na Kiiza ambapo Cannavaro na Msuva walionekana kung’ara kutokana na kupiga penalti zao kiufundi zaidi.
Wakati wachezaji hao wakipewa jukumu hilo lililosimamiwa na Maximo, kwa upande mwingine kocha msaidizi Leonardo Neiva alikuwa akisimamia wale waliochaguliwa maalumu kwa ajili ya upigaji faulo ambao ni Haruna Niyonzima, Andrey Coutinho, pamoja na Nizar Khalfani huku Niyonzima akiibuka shujaa kwa kupiga kiufundi.
Walipofika tamati ya mazoezi yote ndipo Maximo akawaita Tegete, Bahanuzi, pamoja na Kiiza ambao ndio washambuliaji wa kutegemewa wa timu hiyo na kuafanya nao mazungumzo yaliyodumu kwa dakika sita kabla ya kuwaruhusu kuondoka.
Yanga wanataka kulipiza kisasi cha kufungwa mabao 3-1 na Simba Nani Mtani Jembe ya msimu uliopita, ambapo msimu huu mchezo huo utachezwa Desemba 13 Uwanja wa Taifa na kama timu hizo zikitoka sare itabidi kupigiana penalti hadi mshindi apatikane, zoezi ambalo Maximo ameanza kulifanyia kazi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4