Hamis Kiiza aipasua Yanga

VIONGOZI wa klabu ya Yanga wamejikuta katika wakati mgumu kufuatia kuvutana juu ya kuachwa kwa mshambuliaji wake wa kimataifa kutoka Uganda, Hamis Kiiza.
http://api.ning.com/files/yO9SyEbDnuZQdh0M0vFV3QzTpKYRoahPoY-Boyc42SxBr6OWOZPu-fKSRP1wS-A4r1dn-ydGbYUaj7*oS6eB7trfuM1fC7wP/KIIZANEW.JPG
Hamis Kiiza
Hii ni mara ya pili kwa Kiiza kuwekwa kikaangoni kwa kutaka kuachwa kwani katika kipindi kilichopita cha usajili aliponea chupuchupu.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kuwa, Kamati ya Usajili ililazimika kuitisha kikao cha dharura kujadili suala  la mchezaji huyo.
Chanzo hicho kilisema kumeibuka mgawanyiko mkubwa baina ya viongozi wanaounda kamati hiyo, ambapo wengine wametoa mapendekezo ya mchezaji huyo kuvumiliwa hadi msimu huu wa ligi umalizike.
“Ni mara ya pili Kiiza kuleta mgawanyiko kwa viongozi, kipindi cha nyuma wakati anataka kuachwa hali ilikuwa hivi na mwisho wake alibaki kuitumikia timu hii,” kilisema chanzo hicho.
Kamati hiyo inayoongozwa na Seif Magari ilipingana vikali, huku wengine wakidai mshambuliaji huyo kiwango chake kimeshuka hivyo ni vizuri nafasi yake ikachukuliwa na mtu mwingine.
“Wengine wanadai kiwango cha Kiiza kimeshuka ila wapo wanaomtetea na kusema hastahili kuondolewa kipindi hiki, kwani amekuwa na mchango mkubwa wa timu hiyo,” alisema.
Chanzo hicho kilieleza kamati hiyo imeridhia kukutana upya na kujadili suala hilo kabla ya Jumatatu, ili kuhakikisha masuala ya usajili yanakamilika Desemba 14.
Habari za kamati hiyo kupanga kusajili mchezaji mpya Mohamed Traore kutoka Mali zimezidi kushika kasi, huku timu ikiwa na jumla ya wachezaji watano wa kimataifa.
Kiiza ambaye aliponea katika tundu la sindano kutemwa na klabu hiyo,  amebakisha miezi sita kabla ya mkataba wake kufikia tamati.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4