Escrow yamletea balaa Mwenyekiti ccm

MWENYEKITI wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Nyamagana, Raphael Shilatu na Meneja Kampeni wa chama hicho Kata ya Igoma,  Robert Itimbula, jana walizomewa wakati wakijaribu kukitetea chama hicho kutohusika na wizi wa fedha za akaunti ya Tegeta Escrow.
Kauli iliyowaponza viongozi hao wa CCM ni   kuzungumzia suala la uchotaji wa fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow na ubadhirifu wa Sh bilioni 46.5 za Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
Walisema   CCM haihusiki kwa njia yoyote na wizi huo bali ni watu wachache binafasi.http://radiombao.com/wp-content/uploads/2014/01/Chama-Cha-Mapinduzi.jpg
Dalili za kuzomewa ilianza kuonekana mapema   Itimbula alipopanda jukwaani na kujaribu kutambua kuwapo   vyama vya upinzania vilivyohudhuria kwenye mkutano huo wa CCM kwa kuvitaja kimoja kimoja.

Alipotaja  Chadema watu walilipuka  kwa shangwe na vifijo   huku wakionyesha vidole juu kama ishara ya Chadema.

Tukio hilo ambalo lilidumu takribani dakika 15 hadi  kurejea utulivu, liliwafanya viongozi hao kushindwa kuendelea kuzungumza kwa wakati huo.
  Shilatu alisema   CCM itashinda kwa kishindo kwa sababu imefanya mchujo wa wagombea wenye sifa tofauti na ilivyo kwa vyama vya upinzani ambavyo vimewasimamisha watoto ambao hawana uwezo hata wa kusuluhisha ndoa.
“Nataka kuwaelezea mambo ya Escrow na ubadhirifu wa jiji letu uliosababisha kupata hati chafu..., sasa mnapiga yowe, hapa msifanye ushabiki usio na maana… ni vema mkasikiliza ili mpate ukweli, endeleeni na ushibiki huo ambao hautawasadia.
“Serikali ya CCM tumejipanga kuwachukulia hatua wale wote waliohusika ndiyo maana tuliamua kuwaweka hadharani  kupitia Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (PAC) jamii iwajue ni wabadhirifu, kukibwa nawaomba tumieni busara kufanya uamuzi sahihi Desemba 14, mwaka huu,”alisema.

  Meneja Kampeni wa CCM, Itimbula, alisema wamebaini njama za Chadema kuwachukua wanafunzi wa sekondari  na vyuo na kuwaandikisha katika vituo mbalimbali ili kuwapigia kura  ifikapo Desemba 14 mwaka huu na kusisitiza kwamba watawakamata kwa kuwa tayari wamewajua.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4