DIAMOND: Nishachekwa sana kisa Lugha

BAADA ya kurejea nyumbani na tuzo tatu mikononi zilizoamsha furaha ya Watanzania wengi, Nyota wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul ‘Diamond Platnum’, amedai alishawahi kuchekwa sana kisa hajui kuongea lugha ya kiingereza.
Nyota huyo aliyasema hayo baada ya kuzinyakuwa tuzo tano na kuwataka wasanii wenzake kuacha tabia ya uwoga na kujenga mazoea ya kutokuwa na aibu ya kuongea kingereza hata kama hawajui ili waweze kutimiza mafanikio yao.Displaying Diamond kuwasili dar (2).JPG
“Unajua mimi nilichekwa sana ooo Diamond hajui kingereza, sasa kutokana na maneno yao mimi nikawa najitahidi mpaka sasa naingia sehemu mbalimbali ikiwemo mjengoni ‘Big Brothjer’, yani kwa sasa natema maneno mpaka anayenisikiliza anajisikia raha,”.
Alisema ni wakakti wa wasanii wenzake, kuachana na tabia ya majungu, Uwoga, dharau, kasha kutanguliza heshima mbele ili waweze kufanikisha muziki wao ufike zaidi ya alipo yeye hivi sasa.
“Wasanii wakiacha tabia za ajabu ajabu, muziki wa Tanzania utakuwa zaidi ya Nigeria, lakini sasa sisi kwa sisi tunasemana wenyewe kwa wenyewe,  kikubwa ni kujiamini kwa kila mmoja ili muziki wetu usiyumba,”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4