9 wauawa mapigano ya wafugaji Kisarawe
![]() |
Kisarawe |
WATU
tisa wamefariki dunia katika Kijiji cha Kihale wilayani Kisarawe Pwani, baada
ya kuibuka mapigano makali kati ya wafugaji wa jamii ya Kisukuma na Wabarbeigi.
Tukio
hilo lilitokea Novemba 26, mwaka huu ambapo inadaiwa chanzo cha mapigano hayo
ni kijana wa Kibarbeigi kuuawa na vijana wa Kisukuma kwa madai ya wizi wa
ng’ombe.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei, alikiri kutokea kwa tukio hilo na kwamba
hadi jana maiti zote hazijatambuliwa kwa majina.
Alisema
uchunguzi wa kina unaendelea kutambua watu hao walikuwa wanaishi wapi.
“Chanzo
cha mapigano haya kilianza wakati mtu mmoja ambaye ni Mbarbeigi alipoiba mifugo kwa Msukuma mmoja. Hali hii
ilisababisha mtu aliyeibiwa kuwapigia simu wenzake ambao walikusanyika na
kuanza kumtafuta mwizi.
Alisema
baada ya kumpata mwizi walimpiga hadi kufariki dunia jambo ambalo lilionyesha
kuwapandisha hasira Wabarbeigi.
“Baada
ya kuona mwenzao ameua waliamua kujibu mashambulizi dhidi ya Wasukuma ili
kulipiza kisasi… hali hii ilisababisha amani kutoweka ambapo watu walikimbia
ovyo kwa ajili ya kujiokoa,” alisema Kamanda Matei.
Kutokana
na hali hiyo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Pwani, ilifanya juhudi za
kukutana na wafugaji wa jamii ya Wasukuma,
Wamasai na Wabarbeigi ili kuhakikisha
wanasaidiana kuwasaka wahusika.
Mkuu
wa Mkoa wa Pwani, Mwantumu Mahiza alisema amesikitishwa na kitendo hicho.
Kutokana
na hali hiyo, ameliagiza Jeshi la Polisi kuwasaka wale wote waliohusika na
kuwatia nguvuni.
Kwa
upande wake, Mbunge wa Kisarawe, Selemani Jafo (CCM), alisema mauaji hayo ni
mabaya na kuzitaka mamlaka zinazohusika kuchukua hatua haraka za kuwasaka wale
wote walichochea vurugu hizo.
“Nitashirikiana
na Jeshi la Polisi na wananchi kuhakikisha tunarejesha amani, umoja na utulivu
katika vijiji husika,” alisema Jafo.-Mtanzania
Maoni
Chapisha Maoni