Waislamu Ilala kumuombea Rais Kikwete

UMOJA wa Misikiti ya Ilala jijini Dar es Salaam unatarajia kufanya dua maalum  ya kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete itakayofanyika kesho alhamisi katika msikiti wa Taqwa uliopo Ilala, Bungoni.http://www.ibn-tv.com/wp-content/uploads/2011/03/Kaaba2.jpg

Dua hiyo imepangwa kufanyika kuanzia saa mbili usiku baada ya swala ya Inshaa na masheikh mbalimbali wa umoja wa misikiti hiyo pamoja na waumini na wageni wengine wanatarajia kuhudhuria.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Misikiti ya Ilala Sheikh Abdul Wakati, amesema dua hiyo imelenga kumuombea Rais Kikwete ili Mwenyezi Mungu amjaalie afya njema na kurejea katika kuwatumikia watanzania.
“Sisi Umoja wa Misikiti ya Ilala tumeandaa dua hii maalum kwa ajili ya kumuombea Rais wetu apate nafuu na kurejea katika ujenzi wa taifa, tunawaomba waumini wajitokeze kwa awingi katika dua hii ili kuweza kufanikisha azma yetu hii.”

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4