Owino: Hata sielewi nifanyeje

BEKI wa kati na nahodha wa Simba, Joseph Owino raia wa Uganda, ametamka la moyoni na kusema inamuuma sana na anachanganyikiwa kwa kushindwa kuamini matokeo ya ajabu ambayo klabu yake inaendelea kuyapata ikiwa ni sare ya sita, pointi sita, mchezo wa sita na mabao sita.
Owino ndiye mfungaji wa bao pekee la mchezo wao uliopita, waliotoka sare ya 1-1 na Mtibwa Sugar Uwanja wa Jamhuri Morogoro. Beki huyo tegemeo kwenye kikosi hicho alisema: “Inauma sana kuendelea kupata matokeo ya namna hii, sare ya sita.
Nashindwa kuelewa na inashangaza kinachoendelea kutokea kwenye timu yetu, sijui ni nini lakini ndiyo hivyo,”alisema Owino. Lakini mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Mussa Hassan ‘Mgosi’ alisema; “Bado wana nafasi ya kufanya vizuri kwani mechi zilizobaki ni nyingi.”-Mwanasport

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4