Mwambusi: mizengwe,Shutuma vimeniondoka Mbeya City

SIKU chache tu baada ya aliyekuwa Kocha Mkuu wa Mbeya City, Juma Mwambusi kuitosa timu hiyo kwa madai ya kuchoshwa na shutuma zilizokuwa zikitolewa dhidi yake kila kukicha,BINGWA limemsaka na kufanikiwa kuzungumza naye ili kupata undani wa sababu zilizopelekea uamuzi wake huo.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQl3eWljKMRK8nZzuQDEtJIpd78cDNSktrCt0MTNi2k5HM_4B1vJutCEAklpLNsu_7f70-0IeWfRfYzh4FQRjO0qlqMwVebA5Q4f7nts2pK6zaDgUbF0oMnS7k_9yqAJOiYsMrPVzVwEdF/s1600/13.JPG

Mwambusi ambaye alitwaa tuzo ya kocha bora ya msimu uliopita akiwa na kikosi cha Mbeya City amejikuta kwenye wakati mgumu msimu huu baada ya timu hiyo kuboronga kwenye mechi zake hivyo kujikuta ikikamata mkia.
Mbeya City ambayo msimu uliopita ilimaliza ligi ikiwa kwenye nafasi ya tatu,imeshinda mechi moja pekee kati ya saba ilizocheza mpaka sasa,huku ikipigwa nne na kutoka sare mbili.-Gazeti la bingwa limeripoti

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4