Mosoti: Nipo tayari kurejea Simba

http://i2.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2014/03/musoti.jpg?resize=617%2C607
BEKI wa zamani wa Simba, Mkenya Donald Mosoti amesema yupo tayari kufuta kesi na kurejea Simba endapo tu watahitaji huduma yake na kufikia makubaliano kimkataba.
Kauli hiyo aliitoa baada ya kuwepo na taarifa kwamba Kocha Patrick Phiri bado anamuhitaji beki huyo wa kati katika usajili wa dirisha dogo utakaoanza Novemba 15 ili kuboresha safu yake ya ulinzi ambayo inaonekana kuwa tatizo ndani ya kikosi chake.
Jina la Mosoti lilikatwa siku mbili kabla ya dirisha la usajili mpya wa Ligi Kuu Bara kufungwa ambapo nafasi yake ilichukuliwa na mshambuliaji Mganda Emmanuel Okwi na hivyo kuamua kufungua kesi katika Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), kesi ambayo inasimamiwa na wakili wake Felix Majani kwa madai ya kuvunjiwa mkataba wake pasipo makubaliano.
Fifa iliwataka Simba kupeleka vielelezo vyao ikiwemo mkataba baina yao na Mosoti kwa ajili ya kuanza kusikiliza kesi hiyo kwa pande zote mbili lakini viongozi wa Simba walishindwa kufanya hivyo na Fifa sasa wanasubiri kutoa uamuzi wa upande mmoja.
Mosoti (pichani) aliliambia Mwanaspoti kuwa: “Kesi ipo Fifa ambao waliomba mkataba wangu na Simba ili waupitie, wakili wangu Majani aliwapelekea hivyo kinachosubiriwa ni uamuzi tu lakini pia kurudi Simba sio tatizo kikubwa ni kukaa na kufikia makubaliano.”
“Kama wanahitaji huduma yangu mimi sina tatizo ila zitafuatwa taratibu na tukikubaliana kwa pamoja basi hakutakuwa na haja ya kuendelea na kesi hivyo itafutwa,” alisema Mosoti.
Kwa sasa Simba ipo katika mikakati ya kuhakikisha wanaimarisha kikosi chao kutokana na matokeo ya sare waliyoyapata kwenye mechi sita za ligi.
Mabao ya Simba yote yanatokana na beki yao kutokuwa imara kulinda lango lao pale wanapopata ushindi na kuwapa nafasi wapinzani wao kusawazisha.
Tayari Phiri ametaja nafasi anazotaka kuzifanyia maboresho kuwa ni straika, kiungo mkabaji, beki ya kati, beki ya kulia na kushoto pamoja na kipa.-CHANZO Mwanasport

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4