Mauaji ya kutisha Bukoba

JESHI la Polisi mkoani Kagera linamshikilia, Issa Sadiki (49) mkazi wa Itongo, Tarafa ya Nshamba, Wilaya ya Muleba, Kagera kwa tuhuma za kuua watu watatu wa familia moja.http://farm7.static.flickr.com/6022/5984053461_ff2144d749_b.jpgMji wa Buoba
Issa anatuhumiwa kuwaua baba yake, Sadiki Hamis (84) kwa kumtenganisha kichwa na kiwiliwili, mama yake mdogo Zamuda Sadiki (44) na mdogo wake Juma Sadiki (15), aliyefariki akiwa katika Hospitali Teule ya Rubya iliyopo Muleba.
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Henry Mwaibambe, alisema tukio hilo lilitokea juzi saa mbili usiku baada ya kundi la watu wasiojulikana kuvamia familia hiyo na kufanya unyama huo.
Mwaibambe alisema watu hao walimwacha mtoto Aza Sadiki (19) bila kumdhuru, ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Rukondo. Hata hivyo walimnyang’anya simu yake.
https://24tanzania.com/wp-content/uploads/2013/04/b630BUKOBA-AIRPORT.jpg
Alisema kulikuwa na ugomvi wa muda mrefu kwa madai kwamba baba wa familia hiyo alikuwa akitoa huduma kwa upendeleo kwa mke wake wa nne ambaye ni Zamuda.
 “Kwa sababu Hamisi alikuwa na wake wanne, yawezekana wake zake wengine watatu na watoto wao walihisi kuna dalili ya mke mdogo kupewa nafasi kubwa ya kurithi mali pamoja na mwanaye Juma aliyefia katika Hospitali ya Rubya,” alisema Kamanda Mwaibambe.
Aidha alisema chanzo cha tukio hilo ni urithi wa mali na kuongeza kuwa Jeshi la Polisi linamshikilia Issa Sadiki kwa kuhusika na mauaji hayo, na upelelezi unaendelea.-Chanzo MTANZANIA.


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4