Kiongera aanza mdogomdogo

Mshambuliaji wa Simba Mkenya Raphael Kiongera 
MSHAMBULIAJI wa Simba Mkenya Raphael Kiongera amepanga kuanza mazoezi ya gym leo Jumatatu lakini ametamka neno moja tu kwamba atarudi uwanjani kuongeza nguvu ya ushindi katika kikosi chake cha Simba.
Kiongera aliumia goti wakati wa mechi ya kwanza ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Coastal Union na kulazimika kukaa nje ya uwanja kwa wiki nane ambayo ni sawa na miezi miwili na sasa anaendelea vizuri ingawa amesema matokeo wanayopata sasa hayamfurahishi.
Kiongera aliwataka wachezaji wa Simba kutokata tamaa na matokeo hayo bali wanahitajika kupambana zaidi na kuona mwisho wao ni upi kwa kile alichoeleza kuwa katika soka lolote linaweza kutokea, ni kufungwa, kushinda na sare.
“Jumatatu nitaanza mazoezi ya gym ila sijajua nitafanya kwa muda gani, goti langu linaendelea vizuri kwani hata yale maumivu siyasikii kwa sasa, natamani kucheza ili nisaidiane na wenzangu kuhakikisha tunaitoa Simba hapa ilipo, naamini nikipona nitaungana nao.
“Matokeo haya siyo mazuri kwetu na yanasikitisha na kukatisha tamaa, hivyo ni lazima kutafuta sababu ya nini kinafanya matokeo haya yatokee hivi mfululizo ingawa soka ni mchezo wa makosa, ila tukipambana naamini tutafanya vizuri mechi zijazo,” alisema Kiongera.-mwanasport

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4