Coutinho atuma ujumbe mzito

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Mbrazil Andrey Coutinho ambaye kwa sasa yupo nchini kwao kwa mapumziko mafupi baada ya kusimama kwa Ligi Kuu Tanzania Bara, amewataka mabeki wa timu watakazokutana nazo kujiandaa kuchuana naye akiwa katika mwonekano tofauti na ule wa awali.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiiQXQvop_fsMYOtYZyG23Kcn_WaTfv9N3ffL8Mwyr5040SDDSg65bhxzn2e0zOts1GE0jTjQa5j23gGlyWmcYtxznDdMYPl0yk7NiEOKr1qHxcZKSF5ISfaSDDy5WN3aJxRhUzi7o5gI7Z/s1600/COUTINHO+YANGA+SANA.jpg

Mbrazil huyo amesema kuwa baada ya kuwapo hapa nchini kwa takribani miezi minne, kuna jambo kubwa alilojifunza ambalo anaamini akilifanyia kazi huko, mashabiki wa Yanga watafurahi kwani amebaini wachezaji wa Tanzania wanatumia nguvu nyingi zaidi hivyo ili kupambana nao, kunahitajika nguvu za kutosha.
 Ni kutokana na hilo, tangu ametua Brazil, amekuwa akijifua vilivyo kusaka stamina, akihudhuria mazoezi hayo ya viungo katika klabu mbalimbali za mazoezi (gym), lakini pia akikimbia katika maeneo mbalimbali, ikiwamo ufukweni.

“Nafanya mazoezi ya kukimbia kwenye ‘gym’ ili kujiweka fiti kukabiliana na soka la Tanzania linalohitaji nguvu zaidi na kuisaidia Yanga kwenye mechi zinazokuja,” alisema.

Coutinho mwenye uwezo mkubwa wa kumiliki mpira na kupiga adhabu, kona na krosi za nguvu kwa kutumia mguu wa kushoto, amesema kuwa anataka kurejea nchini kivingine na hivyo kufanya kweli kwenye mechi zao zijazo ili kuwafurahisha mashabiki wa Yanga.
  
Alisema kuwa anafahamu mechi yao ijayo itakuwa dhidi ya Simba katika mchezo wa Nani Mtani Jembe ambapo anatarajia kuanza kuonyesha cheche zake siku hiyo akiwa katika sura mpya.
 Mchezo huo wa Nani Mtani Jembe unatarajiwa kupigwa Desemba 12, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.-Chanzo Gazeti la bingwa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4