Azam yatia maguu dili la Mkude

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgUuhljxRimBqmVeyXreYJDprF2LG4MxphUciiy_TsohAJ2GECBZcIfB8ILm4ay0qUHeyml368O7LvTBdk6KeRV-2NTCLvQ2q8gt6Mwru7NkMFZkNWmwJbla0PiM4kDYnYO3Bzq5kH9yAA/s1600/1397179_669015719805454_1383073960_o.jpg
AZAM imeamua kuingilia kati na kumshawishi kiungo wa Simba, Jonas Mkude aliyekuwa akinyemelewa na Yanga atue Chamazi, Mbagala. Mchezaji amebakiza miezi sita katika mkataba wake na Simba ambao bado hawajamuongezea ingawa tayari mazungumzo mepesi yameanza.
Habari zilizopatikana jana Ijumaa zilieleza kwamba viongozi wa Azam walikuwa kwenye mpango wa kumalizana na kiungo huyo lakini hawakuweza kukamilisha mipango yao kwani Mkude yupo kambini na timu yake nje kidogo ya mji ikijiandaa na mechi yao na Ruvu Shooting itakayochezwa kesho Jumapili.
Baadhi ya viongozi wa Simba jana walionekana kuhaha kuhakikisha wanafanya jitihada za kumbana mchezaji huyo ili asisaini mkataba na Azam ambapo wao wamepanga kumalizana naye baada ya mechi hiyo.
“Azam wamepanga kumalizana naye na wapo tayari kwenda kumwingizia fedha kwenye akaunti yake, kinachochelewesha ni kwamba Mkude yupo kambini lakini kuna mazungumzo ya chinichini ambayo yamefanyika juu ya kumalizana na mchezaji huyo,” alisema mmoja wa watu wa karibu na Mkude.
Kiongozi mmoja wa Simba alisema: “Huku (Simba) tumefanya naye mazungumzo tu ambayo yanakwenda vizuri lakini hatujampa mkataba tunasubiri tumalize mechi, Mkude hawezi kuondoka kwani hatua tuliyofikia ni nzuri.”
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgwtMGBSQAIXXu_cXMl-NmrISoAIAflNt0v4dIRvrNAOMnvFZ8ctKfFp6h1fzQ3dEPUljXTt5hp261O8ovPuw2BhfzBm3DcJnCtDeYCdHDs0vjH3sJCl_13RKxA84o_BtaCoKbsQOgZmvM/s1600/mkudee.jpg
Mapema wiki hii Mkude alionekana na gari jipya aina ya GXMark II Grand110 ambalo inadaiwa alipewa na viongozi wake ikiwa ni moja ya mikakati ya kumzuia ili asiondoke lakini kiongozi mmoja wa Simba akafafanua kwamba Mkude alinunua gari hilo kwa fedha yake ambayo alikuwa akiidai Simba.
Msimu uliopita Azam ilikuwa ni moja ya timu iliyomtaka kwa udi na uvumba mchezaji huyo lakini alikataa kwa kuwa mkataba wake ulikuwa bado mrefu.-Credit Mwanasport

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4